Ellis: Banyana Banyana Lazima Ishinde Mechi Zilizobaki Baada ya Kichapo kutoka Tanzania

Kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Afrika Kusini, banyana banyana Des Ellis, amesema kikosi chake sasa hakina nafasi ya kupoteza pointi nyingine baada ya kufungwa mabao 2-1 na Twiga Stars ya Tanzania katika mchezo wa kwanza wa Kundi A wa michuano ya WAFCON 2026 inayofanyika Morocco.

Ellis: Banyana Banyana Lazima Ishinde Mechi Zilizobaki Baada ya Kichapo kutoka TanzaniaMatokeo hayo yamewaacha mabingwa wa Afrika wa mwaka 2022 kwenye presha kubwa, huku wakilazimika kushinda michezo yao miwili iliyosalia dhidi ya Ivory Coast siku ya Ijumaa na Burkina Faso Jumanne ijayo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya robo fainali. Ivory Coast ilianza kampeni zake kwa ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Burkina Faso.

mpira wa miguu, kubeti mpira wa miguu, bashiri soka, soka, beti kwenye soka, odds za soka, bashiri mpira wa miguu, beti za soka, beti mechi za soka, odds za kubeti mpira wa miguu

Licha ya Afrika Kusini kutawala umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, walishindwa kuzitumia ipasavyo, jambo lililoruhusu Tanzania kutumia nafasi zake chache na kufunga bao la ushindi mwishoni mwa mchezo, na kuandika moja ya ushindi mkubwa zaidi katika historia ya soka la wanawake nchini humo.

Ellis alikiri kuwa timu yake ilijigharimu yenyewe kwa kushindwa kutumia nafasi walizopata na kufanya makosa yaliyoigharimu matokeo. “Mabao ndiyo yanayoshinda mechi. Tulijua namna Tanzania itakavyocheza, lakini mabao mawili tuliyoruhusu yalikuwa ya kizembe. Walipata nafasi mbili na wakazifunga zote, wakashinda mchezo. Nilisema kabla ya mechi kuwa ungekuwa mgumu, lakini sisi wenyewe tulifanya maisha kuwa magumu zaidi.”

Ellis: Banyana Banyana Lazima Ishinde Mechi Zilizobaki Baada ya Kichapo kutoka TanzaniaKocha huyo alisisitiza kuwa mechi inayofuata dhidi ya Ivory Coast ni ya lazima kushinda, akieleza kuwa hakuna nafasi tena ya kupoteza pointi. “Mwanzo mzuri ungetupa hamasa, lakini sasa mchezo unaofuata ni kama fainali kabla ya fainali. Ni lazima tushinde, na pia tushinde mchezo unaofuata. Tuna uwezo wa kufanya vizuri zaidi ya tulivyoonyesha leo. Hatuwezi kupoteza pointi nyingine, na kwa kuwa ni timu mbili pekee zitakazofuzu, lazima tutoe kiwango chetu bora.”

Ellis: Banyana Banyana Lazima Ishinde Mechi Zilizobaki Baada ya Kichapo kutoka TanzaniaKatika WAFCON 2026, timu nne zitakazofika hatua ya nusu fainali zitafuzu moja kwa moja kushiriki michuano ya Dunia la Wanawake 2027 litakalofanyika Brazil, huku timu mbili zitakazotolewa robo fainali zikipata nafasi ya kucheza mchujo wa mabara kutafuta tiketi za mwisho. Kwa sasa, kipaumbele kikubwa kwa Banyana Banyana ni kuhakikisha wanavuka hatua ya makundi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.