Azam FC imeweka wazi mustakabali wa benchi lake la ufundi baada ya kuthibitisha kumuongezea mkataba kocha wake mkuu, Florent Ibenge, ambao sasa utamuweka klabuni hapo hadi mwaka 2028.
Uongozi wa Azam FC umethibitisha taarifa hiyo kupitia kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii, ukisisitiza kuwa kocha huyo ataendelea kusalia “nyumbani” Chamazi licha ya uvumi uliokuwepo wa kujiunga na timu ya taifa ya Mali.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Taarifa ya klabu imesema “Florent Ibenge ataendelea kuwa sehemu ya Azam FC hadi mwaka 2028 baada ya makubaliano mapya ya mkataba kati ya pande zote mbili.”
Awali, Ibenge alisaini mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi, lakini mafanikio yake yameifanya klabu kumlinda kwa mkataba wa muda mrefu zaidi kutokana na mchango wake mkubwa.
Chini ya uongozi wake, Azam FC imefanya vizuri katika mashindano ya kimataifa ya CAF Confederation Cup kwa kufika hatua ya makundi kwa mara ya kwanza, huku pia ikiwa nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu ya NBC na pointi 52 ikibakiza mechi tano, sambamba na kutinga nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB.


