Frank Ribery amehusika katika kamba 40 msimu mzima, ametwaa tuzo ya mchezaji bora Bundesliga, amebeba treble pale Ujerumani, kabatini amezifungia medali za UEFA, taji la ligi kuu na DFB POKAL akiwa na Bayern Munich, isitoshe amekuwa mchezaji bora Ulaya.
.
Kule Hispania Ronaldo alikuwa mfungaji bora, alipiga mabao 66 katika mechi zote, Hakutwaa taji lolote zaidi ya kufika fainali ya Copa del Rey. Swahiba wake Lionel Messi alibeba La Liga akirejea kambani mara 42. Hiyo ni 2013.
.
Macho yote yakiwa Paris usiku wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia inatolewa, kila mtu anasubiri Frank Ribery apewe tuzo yake. Maskini ya Mungu hawakujua mfaransa wa watu anaenda kudhulumiwa kama kawaida. Ronaldo aliitwa kama namba moja, Messi namba mbili na yeye akawa namba tatu.
.
Dhuluma tu, walitaka Ribery afanye nini cha ziada? Alibeba kila taji aliloshiriki mwaka huo. Alikuwa mchezaji muhimu zaidi Bayern Munich. Treble aliyotwaa hata Franz Beckenbauer na Gerd Muller hawakuisogelea. Yeye angefanya nini zaidi? Dhuluma tu na dunia haikujalisha. Kwani Ribery ni nani?
.
Watesi wa Ronaldo wangeweza kumtetea Ribery, ila wangezungumza nini wakati wanajua walichokifanya 2010? Wakafanya walichojua, wakampa Lionel Messi tuzo ya mtu. Dhuluma hii.
.
Wesley Sneijder akiwa bingwa wa Ulaya, bingwa wa Serie A na mshindi wa Coppa Italia, akaondoka na Scudetto. Akaenda kuifikisha Uholanzi fainali ya kombe la dunia. Usiku wa tuzo Lionel Messi akawa mchezaji bora wa dunia kisa La liga aliyotwaa.
.
Huyu Sneidjer hakuwa hata tatu bora. Lionel Messi akawa mshindi kwa kigezo cha mabao 47 ya La liga. Iniesta akaja nyuma yake kisha pacha wake Xavi Hernandez katika nafasi ya tatu. Ndiyo hivyo. Golden, silver na Bronze medals zote zikamwagwa Barcelona. Sneijder wa watu akachinjiwa baharini.Hii dhuluma nani atatusaidia?
.
Tunakubali mlituletea chakula ambacho hatukuwahi kukionja kabla ila hatukujua kama mnatulisha hadi saza mlizowaibia maskini. Siwataji kwa majina. Msipolipwa na Wanadamu mtalipwa hata na historia.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
magdalena
mh ayo maneno ya kuzusha ata siyaamini nikiwa kama shabiki
Lydia Emmanuel Magoti
Hayo ndio maneo yasiyo takiwa kuongerewa maneno yasio yauwakika namaneno yakumpa mtu sifambaya
Angelina
Zuluma sio nzuri
Salma ngende
Hakuna ukweli wowote
Fatuma kasomo
Duh sio poa
Antony Luseno
Swala la mchezaji bora uwa linahusishwa na mambo mengi sana ambayo ndo uzingatiwa
Mariam mtandama
Duuuh
Adelta
Ni vizazi Bora vilivyotokeah kwny soka hv sasa
Sania
Sio poa kabisa
Ester jackson
Mambo haya huwa yanatokea sana
Sarah
Duu dhuluma mbaya
Shakila mrope
Dhuruma sio nzuri kabisa
Mwajumah
Duuh sio pow
Tatu
Sio poa
Fatina mfingi
Duuh mbona mamb hay awaendan nayo
Elika
Hiyo cauple naielewa sana
lombo
mmh
Rehema
Good new
Hopemwaikuka
Makubwa haya
Povel
Vizazi bora vilivyotokeah kwny ulimwenguni wa kabumbu
aisha
Majanga hayo
Saupha mohamed
Dhuuuu
Tahiya
Duuh
Issa
Ronaldo na mess ni wachezaj ambao hawatawah kutokea ulimwenguni
Sauda
Siyo poa
Janeflora malisa
Duh
warda
Habari poa sana