Timu ya Taifa Stars ya Tanzania leo imepoteza kwa kufungwa bao 1-0 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Burundi uliochezwa Uwanja wa Mkapa.
Kwenye mchezo wa leo ambao mgeni rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kipindi cha kwanza timu zote mbili zilitoshana nguvu baada ya kwenda vyumba vya kubadilishia nguo wakiwa hawajafungana.
Kipindi cha pili mambo yalizidi kuwa magumu kwa timu zote mbili ambapo Stars ilijaribu kufanya mashambulizi yalishindwa kuzaa matunda na Burundi ilikuwa ya kwanza kupiga shuti la kwanza ambalo lililenga lango kipindi cha pili.
Bao pekee la ushindi lilipatikana dakika ya 84 kupitia kwa Said Ntibazonkiza na kuwafanya Burundi kuibuka na ushindi ugenini.
Simon Msuva nyota wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars amesema kuwa haikuwa bahati kwao kwa kuwa walipambana ili kupata ushindi ila mambo yalikuwa magumu kwao.
Stars ilimaliza dakika 90 ikiwa pungufu baada ya kiungo mkabaji Jonas Mkude kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 78 kwa kuwa alikuwa alionyeshwa kadi mbili za njano.
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.
magdalena
taifa stars walionesha juhudi za hali ya juu ila bahati haikuwa kwao
Elika
Ni kujipanga upya kipindi kijacho
Zeiyana
Taifa stars wametuangusha watanzania kwa kweli hatukutegemea matokea yale
Fatina mfigi
Jipangeni upya bahat haikuwa upande wetu!
Adelta
Waongeze juhudi na mazoezi yakutosha ili msimu ujao wafanye vizuri
Ester jackson
Taifa stars wanajua kucheza mpira tena vizuri tu ingawa mkude simba alituangusha alivyo pewa kadi nyekundo hapo tulicheza pungufu na kuonyesha uwezo wetu japo tulifungwa ila mpira ulikowa bomba
Lydia Emmanuel Magoti
Timu yataifa Stars ilionesha ushilikiano kwakweli walijitaidi mpaka izo dakika zilizo salia kupigwa goli moja dakika za majerui walionesha ushindani kwakweli ilandio ivyo matoke kupigwa 1-0
MnonganeJR
Tanzania tulistahili kufungwa.
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
aisha
Taifa stars sijajua walikwama wapi maana juhudi zao tuliziona
Salma ngende
Sifa ya Wa tz tunajuwa kuongea kuliko vitendo kwenye upande Wa michezo tuna safari ndefu
Rose kapinga
Kuteleza sio kuanguka bado wana nafasi ya kujipanga upya!!!
Tatu
Mechi ilikuwa nzuri wachezaji walijitahidi kucheza kwa hali ya juu
Mwajumah
Asiye kubali kushindwa sio mshindani na ndio hali iliyotukuta taifa stars ila juhudi tulizionyesha bahat tu haikua kwetu
Dorophina
Inatakiwa kujipanga taifa stars kwa mechi zingine hiyo inabidi wakubaliane na matokeo
Angelina
Taifa stars wamezingua
Amiri Kayera
Stars wamechez vizur Ila umaliziaj ni mbaya
Hidaya
Tumetia aibu jamani kufungiwa nyumbani
Saupha mohamed
Sasa wajiange upyaa
Rehema
Daa! Asante kwa taarifa
Ernest
Timu yetu ya Taifa inatakiwa ijipange zaidi, sio mwanzo mbaya
Issa
Stars bado sana kisoka inabid timu ikae muda mrefu waelewane
Shani
Timu inatakiwa ikae pamoja kwa muda ili wachezaji wafamiane
Sabrina
Taifa stars wameniangushaa
Sauda
Wafanye mazoezi ya kutosha
Venerose
Taifa star wapo vinzur ni bahati mbaya
Neema
Taifa star wanahitaji mazoezi mazito
Genia Sikaluzwe
Mazoezi Yana hitajika mazito
Caroline
TZ tunakwama wapiii
Gabriel
Taifa stars wametuangusha
Hopemwaikuka
Sawa