Nadhani PSG wamejifunza siku nyingine, usipotumia nafasi zako basi uwe tayari kupoteza. Walikuwa timu bora uwanjani kwa dakika 60. Walikaba vema, walitengeneza nafasi ila hawakujua namna ya kuuweka mpira kambani. Wangeweza kuongoza mabao mawili kabla Bayern Munich hawajapata bao.
Njia waliyotumia PSG kumdhibiti Sergie Gnabry, ni njia hiyohiyo waliyoitumia Bayern Munich kumdhibiti Kylian Mbappe. Hakikisha yupo mtu karibu kabla hawajapata mpira. Sikushangaa kutokuwaona Joshua Kimich na Juan Bernat wakipanda.
Coman alizikuta akili zake kwenye vyumba vya kubadilishia nguo walipoenda mapumziko. Kwa kile kipindi cha kwanza alikuwa machachari badala ya kuwa hatari. Pengine hakutegemea kuwepo kwenye karatasi ya majina ya wanaoanza. Aliporejea kipindi cha pili, akaelewa maeneo ya kusimama ili aisadie timu kushambulia zaidi. Kwa dakika 25 za kwanza za kipindi cha pili, alikuwa mchezaji hatari zaidi uwanjani.
Neymar anazidi kutufanya tuamini kuwa Ronaldo na Messi hawatokei ndani ya hii dunia. Siku ambayo alitakiwa asimame kama mchezaji mkubwa kuitetea PSG, yeye alipotea kabisa. Hakuhusika sehemu kubwa ya mchezo. Ni kama alikuwa na mchezo wake peke yake. Kitu pekee alichowasaidia PSG leo, ni kulia baada ya mechi.
Acha tumalize tu na Thiago Alcantara. Yule mhispaniola anajua bwana. Ni kama anaona mara tatu zaidi ya binadamu wa kawaida. Njia anazopitisha pasi, namna anavoendesha timu, misuli yake wakati anakaba. Absolutely heavenly! Alcantara mtu mmoja na nusu.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.
Sadick
Rio Ferdinand aliwaambia Man U baada ya kutolewa na Sevilla kwamba unaposhindwa kutumia nafasi unazopata tarajia kuadhibiwa na ndicho walichokutana nacho PSG#meridianbettz
Saupha mohamed
PSG walikua wanafanya vizuri kipindi cha kwanza …wamekuja kaharibu mwishoo kabsa ..kwr mpira dk90
Mwanahamisi
Gud news
Antony Luseno
Kwa atua waliofika ya fainali wamehitaidi sana
Issa
Psg ni kama washambuliaj wao hawakuwa na umakini wakifik golini kwa bayern chansi za wazi walizopata zilikuwa zinamaliza matokeo mapema
Ernest
Watu wengi jana tulikuwa na Imani juu ya PSG kutwaa ubingwa pia walianza vizuri kipindi cha kwanza lakini umakini tuu ndio uliwagharimu PSG na kupokea kipigo cha goli moja lakini pongezi nyingi ziende kwa Kipa Neuer kwa kusave mipira ya hatari kutoka kwa Neymar na Mbapper jana
Khadija
kipigo cha goli moja lakin pongezi nging ziende kwa kipa neuer kwa kusevu mipira mingi ya hatari kutoka kwa neymar na mbappe jana#meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Mwenendo wa PSG ulikuwa mzuri Ila ndio mpila kwaio wamejitaidi Sana goli moja sio mbaya Ila PSG walikaza Sana mpaka kufungwa goli moja wamefanya kaz kwampi ule walio kuwa Wana ucheza PSG ulikuwa mzuri nibati mbaya tuu
felister
psg bahati haikua ila walijitahidi sana kucheza mpira
magdalena
PSG mpira waliupa sana ushirikiano ila tu mpira ndo haujawapa ushirikiano wajipange kwa msimu ujao tu
Fatuma kasomo
Sema psg walijitahidi
Shan
Psg ni Kama hawakuwa makini kwa mechi ya jana bahati haikuwa kwao
Gabriel
Gemu hii ilikuwa ya ushindan mkubwa sana kiukwel kwa pande zote mbili
aisha
Psg walijitahidi sana sema bahati haikua ya kwao
Theckla
Mechi ya Jana ilikuwa ina raha yake
Furahav
Alkantara ni noma sana.
Povel
Walichezah vzr walitengenezah nafas nyng sema hawakuwah na bahati katika mchezo ule congrat Bayern championππππ
Hope mwaikuka
Gemu ilkua ngumu kwa wote ila ndo lazima mshnd apatkane
Rose kapinga
PSG wamepambana ila bahat haipo kwao!!!
Amiri Kayera
Psg haikuwa bahat yao
Genia Sikaluzwe
Mechi ya Jana ilikuwa ngumu Sana kwa psg
Shafii
Siku zote mpira ni mchezo wa makosa unapofanya makosa ndipo mwenzako anatumia makosa yako kukuadhibu PSG wajipange kwa msimu ujao.
Theonestina
PSG wajipange kwa msimu ujao
Zeiyana
Siku zote waenga wanasema mkamia maji hanywi..!kwa kuangalia pale PSG mbappe alikua na shauku sana ya ubingwa lakini mwisho wa siku hatukuona mbwe mbwe zake kakutana na wanaume wamemana ukutani big sana Bayern
Sabrina
PSG Jana wametaga Bhana wamezingua sana
Frank P
Nilishangazwa sana jana na how marko verrati fundi hakuwepo etii
David Pere
Watu wengi jana tulikuwa na Imani juu ya PSG kutwaa ubingwa pia walianza vizuri kipindi cha kwanza lakini umakini tuu ndio uliwagharimu PSG na kupokea kipigo cha goli moja lakini pongezi nyingi ziende kwa Kipa Neuer kwa kusave mipira ya hatari kutoka kwa Neymar na Mbapper jana
Rehema
Wamezigu sana pSG
Dorophina
Psg bahati haikuwa yao ndio maana wamepoteza gemu
Sauda
Hapo walipofikia wamejitahidi sana
Caroline
Poleni Sana P.SG haikua riziki
Nasra
Pole sana kwa PSG
Fatina mfingi
Psg bahat haikuwa kwao lakini walicheza Sana mpira
warda
Mpira ulichezwa Lakin Lazima apatikane Mshindi tu