Mabingwa wa Bundesliga wameungana na ndugu zao Borussia Dortmund na RB Leipzig katika kutangaza kutounga mkono mashindano mapya ya Ulaya.
Siku ya Jumapili timu 12 kutoka England, Spain na Italia zilithibitisha kwamba zinajiandaa kujiunga na mashindano ya European Super League ambayo yameundwa kwaajili ya kuleta upinzani kwa Champions League.
Katika taarifa CEO wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alithibitisha kwamba klabu yake haitashiriki na badala yake watakuwa na mtizamo wa kurekebisha Champions League.
“FC Bayern haitashiriki katika mpango wa Super League ,” Rummenigge alisema. “Tuna hakika kwamba muundo wa sasa katika mpira wa miguu unahakikisha msingi wa kuaminika.
“FC Bayern inakaribisha muundo mpya katika Ligi ya Mabingwa kwa sababu tunaamini kuwa ni hatua sahihi kwa maendeleo ya soka la Ulaya. Duru ya awali iliyobadilishwa itachangia msisimko zaidi na hisia katika mashindano hayo.
Wakati vilabu vinapotangaza mipango yao ya Super League, UEFA pia ilithibitisha Jumatatu kwamba kutakuwa na Ligi ya Mabingwa iliyorekebishwa kuanzia 2024.
Muundo mpya utaona timu 36 zinashiriki katika muundo wa ligi moja kuchukua nafasi ya hatua ya makundi. Kila timu itacheza jumla ya michezo 10 nyumbani na ugenini, na nane bora zinafuzu moja kwa moja kwa 16 bora na zile zinazomaliza kati ya tisa na 24 kushindana katika hatua mbili za kucheza ili kuamua nani mwingine anayeingia hatua ya mtoano.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.
warda
Bayern wanaogopa kuchoka
[email protected]
Bayern wako juu
Khadija
Banner wapo vzr sana
dorophina
Bayern mbona kama wanakimbia mashindano hayo
Magdalena
Bayern Munich wanaogopa kwenda uko ili wasijichoshe
Elika
Pole yao
aisha
Bayern nawakubali sana
Venerose
Mmmh mbona kazi ipo
Lydia Emmanuel Magoti
Bayern nawakubali
Sarah
Pole yao