Messi Anavyotukumbusha Mungu Yupo

Nimesikia maajabu mengi sana duniani ikiwemo mchanga unaotembea katika hifadhi ya taifa Ngorongoro. Nimesikia juu ya miti inayotembea ndani ya msitu mkubwa wa Amazon. Unajua bado siamini kama ipo chemchem inayotoa maji ya moto chini ya ardhi? Hii ni miujiza ya Mungu tu.

Mbona picha hapo juu ni ya Messi na stori inayoendelea hapa ni ya Mungu?? Je ninataka kumfananisha Messi na Mungu?? La! Kamwe Siwezi kushiriki dhambi ya kumuita Messi Mungu.

Picha ya Messi akinyoosha mikono na kuangalia juu unaiona kila anapofunga. Ni kwasababu anakumbuka matatizo ya kukua aliyokuwa nayo utotoni. Barcelona wakamsaidia akapona. Lakini kamwe hajawahi kuamini kuwa Barca ndiyo wamemsaidia. Anaamini ni Mungu tu. Licha ya hayo anaamini ni Mungu aliyempa kipaji, si ujanja wake.

Hiyo ndiyo sababu haya maandiko yamekuja muda huu. Hiyo ndiyo sababu picha ya Lionel Messi ipo hapo juu. Wakati unasherekea mwaka huko ulipo, kumbuka kumshukuru Mungu alipokutoa. Labda asubuhi nitaweka picha ya Sadio Mane akisujudu halafu nitaandika mengine. Huyu Messi wa leo ni nani?

Sadio Mane Akisujudu Uwanjani

Maajabu ya miguu yake yanaanza kusimuliwa Paris kwenye tuzo za ‘Ballon d’or’ 2005. Gaucho alipopewa tuzo ya mchezaji bora wa dunia alisema, “Hii tuzo inasema mimi ni bora duniani, ila ninawaambia ukweli mimi sio bora hata ndani ya Barcelona.”

Dunia ilimuona Gaucho kichaa. Yaani kuna mchezaji bora Barcelona zaidi yako? Nani? Xavi Hernandez au Samuel Eto’o. Si dokta Kashushu Leakey wala mzee Habibu Msonjo aliyeelewa maneno yale.

Ila Gaucho alishamtazama Messi pale La Masia, kisha akacheza naye El Clasico akamuona mtoto wa miaka 17 anavyopangua ukuta wa Sergio Ramos, Ivan Helgera, Roberto Carlos na golini alikuwepo Iker Casilas, Gaucho akakubali huyu dogo ni ‘moto na mkaa wake’.

Leo hii mikono ya Messi imenyanyua makombe zaidi ya 33. Miguu yake imevunja rekodi ya mabao ya mfalme wa soka Pele. Shingo yake imetundika medali zaidi 40. Sura yake imepigwa picha na ballon d’or sita. Kabatini kwake ana tuzo zaidi ya 80 na jezi zake mbili tu, Barcelona na Argentina.


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?

SOMA ZAIDI

23 Komentara

    Kweli mungu yupo na anaona kila kitu
    Kinachofanyika chini ya dunia

    Jibu

    Messi noma

    Jibu

    Mungu yupo.na ndo Kila kitu

    Jibu

    Kweli mungu yupo tena ni mmoja tu hakuzaa wala hakuzaliwa

    Jibu

    Leo ni moto sana

    Jibu

    Kweli mungu yupo nandio Kila kitu kwetu

    Jibu

    Kweli mungu ndio muweza wa kila jambo

    Jibu

    Messi kiboko mungu yupo kweli

    Jibu

    Mess fundii

    Jibu

    Mess kidume jeuri

    Jibu

    Messi mwamba anayeishi sasa aje kumalizia soka Uingereza tupate udambwi dambwi wake kwenye ligi ya dunia EPL

    Jibu

    Messi jembe la kazi

    Jibu

    Messi baba lao

    Jibu

    Salute kwa Mwandishi imetulia sana hii

    Jibu

    God over everything

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Inapendeza km anamkumbuka Mungu

    Jibu

    Kweri kabisa Messi mwamba wa miamba anajua

    Jibu

    Mungu kwanza,Messi namkubali

    Jibu

    Messi kama messi namkubali

    Jibu

    safi

    Jibu

    Kweli kabsa mungu ndio kila kitu

    Jibu

    Lazima umwamini Mungu kwanza

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.