Italy wanapigwa 4-0 ndani ya Kyiev Ukraine. Wameshindwa kabisa kujibu maswali magumu wanayoulizwa na Hispania. Watafanya nini mbele ya watoto wanaowaka moto mguuni? Katikati yupo Sergio Busquets, Xavi Hernandez, David Silva na Xabi Alonso. Utawaambia nini? Hapo Andres Iniesta amesogezwa mbele, Italy wamedanganywa ni mshambuliaji. Watoto wa Hispania hawaelewi kitu, wanapika tu sambusa uwanjani. Wanagonga tu. Hiyo Hispania, acha kabisa.
Hispania walikuwa na kiburi cha binadamu mmoja katikati ya dimba aliyezibeba akili zao, akaibeba falsafa yao na akabeba ramani yao. Alipiga pasi zaidi ya nusu za pasi walizopiga Italia. Bado alitoa assist mbili. Alikuwa kitanzi kwenye shingo ya Italia. Sorry, namzungumzia Xavier Hernandez Creus.
Baada ya bao la Juan Mata, Ilibidi Iker Casilas asogee hadi katikati ya uwanja kuwaombea Italy msamaha. Casillas akamnong’oneza Xavi, “Hii ni Italy, mabingwa wa dunia mara nne, isitoshe wana Andre Pirlo katikati ya uwanja na gwiji Gianluigi Buffon langoni, sitataka kuwaona wakifungwa tano, tafadhali inatosha. Wasimamishe vijana”. Hiyo ndio ikawa ‘pona’ ya Italy.
Usisahau hiyo ni fainali ya ‘EURO 2012’, wanaitetea tena kwa mara ya pili. Ni hapahapa Kyiev walivunja rekodi ya kupiga pasi nyingi katika mchezo mmoja. Wakati wanawakung’uta Ireland katika mchezo wa makundi, Hispania walipiga pasi 857, Xavi na rafiki yake Iniesta wakipiga nyingi zaidi ya timu nzima ya Ireland. Iniesta akawa mchezaji bora wa mashindano, ila Xavi alikuwa mchezaji bora mashindano yaliyopita ya 2008. Wakabadilishana tuzo kama walivozoea kubadilishana namba za jezi. Vaa nane klabuni, mimi niivae timu ya taifa. Wale watu.
Muulize hata Frank Lampard anawajua. Alipoulizwa kiungo mgumu kuwahi kukutana nae, alishindwa kuchagua akasema tu Xavi na Iniesta. Sijui yupi mgumu zaidi, ila hao wawili. Sijawahi kuona wachezaji wanaoelewana uwanjani kama wao. Huwezi kuwasogelea, huwezi kuwakaba, huwezi kuwakimbia, wanakuchanganya tu. Hadi sir Alex Ferguson analijua balaa lao. Wakati Barca wanampiga 2011..
ITAENDELEA..
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.
Khadija
duh!!!mambo moto
Sabrina
Wako vizuri sana
Amiri Kayera
Viungo Bola kuwahi kutokea dunian
Hope mwaikuka
Aisee! Ilkua balaa
neema hassan
Asante kwa makala
Genia Sikaluzwe
Ahsant sana meridianbet kwa makala
Dorophina
Viungo bora kabisa wapo vizuri sana na wanaviwango vya hali ya juu
Gabriel
Waliofanya vzur sana kipind kile ila still now wamechoka
Fatina mfigi
Wapo vizur hatar!!
Mwanahamisi
Wako vizuri sana
magdalena
walikuwa nguli sana kipindi iko
Sauda
Viungo bora duniani
Mwajumah
Wako vizuri sana
Nasra
Safii sana kwao
Shani
Update nzuri!
Caroline
Wapo vizuri hao
Sadick
Ilikuwa raha kuona soka lile la spain kama vile play station#meridianbettz
Neema
Duuu wako bomba sana
aisha
Viungo makini sana hawa walikinukisha kipindi hik
Khadija
Habari njema
Hidaya
Kipindi hicho ndio walitamba
Povel
Duh mambo yalikuwah ni moto Sana enzi hzo
Saupha mohamed
Ilikua nomaa
Issa
Viungo bora kuwahi kutokea pale spain
Rehema
Habari njema
David Pere
Waliofanya vzur sana kipind kile ila still now wamechoka
Tahiya
Walifanya makubwa kwenye ulimwengu wa soko sema hawakuwa na bahati
Tatu
Wameweka history nzuri
Ernest
Kizazi cha Xavi na Iniesta bado hakina warithi ndani ya Spain
felister
viungo bora hawajai kutokea duniani
Furahav
Balaaa sana.
Ester jackson
Walikuwa vizuri ila hasaivi hana kitu kabisa
warda
Hawa jamaa wote wakali