Kunako anga la mpira wa kikapu, LA Lakers wametwaa ubingwa wa NBA 2019/20. Ushindi katika mchezo wa 6 umewatosha Lakers kubeba ubingwa baada ya miaka 10.
Ama kweli kukata tamaa ni jambo ambalo halipaswi kupewa nafasi, kuamini katika muda muafaka ni kitu sahihi. LA Lakers wamesugua benchi kwa miaka 10 bila taji la NBA na sasa ukata wao umemalizika 2019/20.
LeBron James na Anthony Davis watabaki kuwa mashujaa wa LA Lakers vizazi na vizazi baada ya kuisaidia timu hiyo kubeba taji la NBA msimu huu.
Uelewano wao uwanjani na kujituma kwao kulikuwa ni chachu ya mafanikio ya Lakers msimu huu. Walicheza kwa kujiamini na kuisaidia timu yao kwa ujumla, katika kila hali walionekana kuwa pamoja na kuhakikisha lengo lao linatimia.
Ushindi wa pointi 106-93 dhidi ya Miami Heats, ulitosha kuwapa Lakers taji la 17 la NBA. LeBron James akajibebea taji la Mchezaji bora wa fainali (Most Valuable Player -MVP) baada ya kupachika pointi 28, alitoa pasi 10 za magoli na kucheza mipira 14 iliyokufa.
Ushindi huu wa LA Lakers, umewapa nafasi ya kuwa sawa na Boston Celtics kama timu zilizobeba mataji mengi ya NBA.
“Hii inamaana kubwa sana kwenye timu hii Wakati ninajiunga na timu hii, nilimwambia raisi (Jeanie Buss) ninakwenda kuirudisha timu katika nafasi yake inayostahili.
“Tunahitaji heshima yetu. Rob [Pelinka] anahitaji heshima yake, kocha [Frank] Vogel anahitaji heshima yake, timu yetu inahitaji heshima yake na mashabiki wote wa LA Lakers wanahitaji heshima zao.
“Na mimi pia ninahitaji heshima yangu.” alisema LeBron James.
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.
magdalena
nilijua tu hamtoniangusha na mmefanya kweli pongezi kwenu vijana wa NBA nawakubali tangu mwanzo
Zeiyana
Hanajituna sana lebron james pale la Lakers nafasi yake kama messi Barcelona
neema hassan
Pongezi kwao
Ester jackson
Hongera yao
Lydia Emmanuel Magoti
Pongezi zao Lakers
aisha
Wanasitahili pongezi sana
Angelina
Safi lakers
Tatu
Lakers walikuwa wazuri toka mchezo ulivyoazs
Mwajumah
Hongera yao
Dorophina
Pongezi kwao lakers
Amiri Kayera
Wamestahili maan wamekua Bola msim huu
Hidaya
Pongezi kwao
Sadick
Bravo LA LAKERS, Bravo Lebron James. Tangu asitaafu Kobe Bryant hakupatikana mtu mwenye uwezo aina yake kuirudisha timu kwenye enzi za ushindi
Sabrina
Weee hongera sana LA LAKERS kazi nzuri
Ernest
Lakers wamestahili, Pongezi kwao
Sauda
Safi sana Lakers
Neema
Hongera yao
Caroline
Hongera yaoo