LeBron James Aivusha LA Lakers Kunako NBA Play-Offs

Michezo ya Regular Season kunako NBA imekamilika na sasa macho yote ni kwenye Play-Offs, LeBron James aokoa jahazi la Lakers akitoka kwenye majeruhi.

LA Lakers walikuwa uwanjani kuchuana na Golden State Warriors katika mchezo wa Play-in tournament. Huu ni mchezo ambao uliozikutanisha timu 2 zenye upinzani mkubwa kwenye NBA na safari hii zilikuwa zinachuana kuwania nafasi 2 zilizobaki kwenye msimamo wa Western Conference.

James akipachika mpira wa pointi 3 muhimu kwa Lakers vs Warriors.

Baada ya kukosekana kwenye michezo kadhaa ya Laker, LeBron James alipachika pointi 3 muhimu zikiwa zimesalia sekunde 58 mchezo huo kumalizika. Ushindi wa pointi 103-100 umewatosha Lakers kufuzu hatua ya mtoano na sasa watachuana na Phoenix Suns katika mchezo wa kwanza siku ya Jumapili.

Licha ya Stephen Curry kupachika jumla ya pointi 37 kwenye mchezo huo, hazikuwatosha Warriors kufuzu na badala yake watachuana na Memphis Grizzlies kwenye mchezo ambao mshindi ataungana na timu zingine 7 zilizofuzu kucheza NBA Play-Offs kwa upande wa Western Conference.


UNAWEZA KUWA MILIONEA WAKATI WOWOTE!

Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.

BASHIRI SASA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.