Ni habari njema kwa wapenzi wa mpira wa kikapu na timu ya LA Lakers. Shujaa wa Lakers – LeBron James, yupo mbioni kuongeza mkataba wa miaka miwili.
Taarifa za kuongeza mkataba mpya zimetolewa na wakala wa LeBron James ambaye aliiambia ESPN mkataba huo utamalizika 2022/23 ambapo pia James atakuwa anatimiza miaka 20 ndani ya NBA.
Mkataba mpya wa James utakuwa na thamani ya pauni milioni 63. Mwishoni mwa mkataba huu utakuwa ni mwanzo mwa safari ya mtoto wa James (Bonny – anamiaka 16 kwa sasa) ambaye atakuwa tayari kuingia kwenye NBA baada ya kumaliza masomo yake.
James aliisaidia Lakers kutwaa ubingwa wa NBA mapema mwezi wa Oktoba na alibeba tuzo ya MVP katika mchezo wa fainali. LeBron James anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji wa NBA aliyebeba mataji ya ligi hiyo akiwa na timu 3 tofauti.
Kwa upande wa kiuchumi, kufikia mwishoni mwa mkataba wake na Lakers, James atakuwa na pato linalokadiriwa kuwa ni pauni milioni 324.
Msimu mpya wa NBA 2020/21 utazinduliwa rasmi Disemba 22 ambapo LA Lakers watachuana na LA Clippers katika mchezo wa kwanza.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
Sabrina
Itakua poa sana jeshi akidondisha saini yake hapo ilikuendelea kusalia hapo LA Lakes
Magdalena
Kila LA kheri kwake
Rahma
Kila lakheri uko uendapo
Hopemwaikuka
Lebron bado mchango wake unahtajka hapo
Adelta
Lebron james ni mtu mwenye uwezo mkubwa na anakubalika
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Caroline
Lakers timu kubwaa
Dorophina
Kila lakheri james haendelee kuwakilisha Lakers
Issa
Le bron ni safi sana
Janeflora malisa
Vzr
Saupha mohamed
Kila LA kheri
Samira
Hao ndio wenye lakers yao all the best James
Mariam mtandama
Safi
Fatina mfingi
Nice
aisha
Imekaa powa sana
warda
Hongera yake