Kuna msemo wa kiswahili unasema ‘sheria ni msumeno, inakata pande zote’. Ndicho kilichowakuta Milwaukee Bucks kunako NBA.
Milwaukee Bucks wameingia matatani baada ya kuvunja sheria ya NBA ya kuzungumza na wachezaji huru, mlengwa akiwa ni Bogdan Bogdanovic.
Bucks waliripotiwa kuingia makubaliano na Bogdanovic mwezi uliopita licha ya mchezaji huyo kuamua kujiunga na Atlanta Hawks baada ya kufanya vizuri alipokuwa na Sacramento Kings.
NBA wamegundua kuwa Milwaukee Bucks walivunja sheria ya muda unaoruhusiwa kufanya mazungumzo na mchezaji huru, hii imewagharimu Bucks ambao watakosa nafasi ya kuchaguliwa kwenye mzunguko wa pili 2022.
Taarifa kutoka NBA imeripoti “ligi ilifanyauchunguzi kama Milwaukee walifanyamazungumzo na Bogdanovic au wakala wake kuhusu mkataba wa mchezaji huru kabla ya muda unaoruhusiwa.
“Uchunguzi umethibitisha maongezi hayo kufanyika na ni uthibitisho wa kuvunjwa kwa sheria za NBA.
“Adhabu imezingatia ushiriki wa Bucks kwenye uchunguzi, kukosekana kwa ushahidi wa mkataba wowote wa awali ambao hauruhusiwi kwenye makubaliano ya mkataba kati ya Bucks na Bogdanovic na uhalisia kuwa timu haikumsajili Bogdanovic.”
Milwaukee Bucks watauanza msimu mpya wa NBA kwa mchezo dhidi ya Boston Celtics kesho Jumatano.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Saupha mohamed
Good news
Asia Abdy
Duuh hatari
Lydia Emmanuel Magoti
Duu sio poa
David Pere
NBA wamegundua kuwa Milwaukee Bucks walivunja sheria ya muda unaoruhusiwa kufanya mazungumzo na mchezaji huru, hii imewagharimu Bucks ambao watakosa nafasi ya kuchaguliwa kwenye mzunguko wa pili 2022.
Fatina mfingi
Duuh pole yake
farida ahmad
Nouma Sana
Mariam mtandama
Pole yake
Issa
Bucks ijifunze kuendana na wachezaji
Sarah
Pole yake
Hopemwaikuka
Next time ataheshimu sheria
Tatu
Sio poa
warda
iko poa