Muendelezo wa NBA Eastern Conference umefikia patamu, baada ya kupoteza mchezo wa kwanza, Milwaukee Bucks wamerejea mchezoni.
Hawks waliingia kwenye mchezo wa pili wakiwa wametoka kuwafunga Bucks kwenye mchezo wa kwanza. Mambo yalibadilika, Giannis Antentokoumpo apeleka kilio Atlanta.
Antentokoumpo alipachika jumla ya pointi 25 katika ushindi wa pointi 125 -91 dhidi ya Hawks. Ushindi wa Bucks unabadilisha taswira ya matokeo ya mchezo huu na sasa ni 1-1.
Mchezo wa 3 kati ya Bucks vs Hawks kwenye fainali ya NBA Eastern Conference, utachezwa Jumapili hii.