Ni mwendo wa vipigo na vicheko kunako Ligi ya NBA nchini Marekani. Rekodi zinawekwa na kuvunjwa kila iitwapo leo. 2020/21 hakika mambo ni moto!
Licha ya Golden State Warriors kutokuwa na msimu mzuri, Stephen Curry ameendelea kuwa bora na kuonesha uwezo wake binafsi katika kuitumikia timu hiyo. Warriors walikuwa uwanjani kuchuana na Milwaukee Bucks alfajiri ya leo.
Mchezo uliomalizika kwa Warriors kuibuka washindi kwa pointi 122-121, umewapunguzia machungu ya kupoteza michezo mfululizo wakati huu ambao walikuwa wameshapoteza michezo 7 kati ya 8 waliyocheza kwa siku za karibuni.
Curry alipachika jumla ya 41 huku akifunga pointi 30 katika kipindi cha pili. Warriors walipindua matokeo wakiwa wamezidiwa pointi 10 na zimesalia dakika 4 mchezo kumalizika.

“Tulihitaji ushindi ili tujisikie vizuri. Ushindi unatuongezea uwezo wa kujiamini na unatusaidia kuendelea kutengeneza utambulisho wetu.” alisema Curry.
Kwa hali ilivyo kwa sasa, Warriors wanashika nafasi ya 10 kwenye msimamo wa NBA – Western Conference na hawapo kwenye nafasi ya kucheza play-offs wakiwa wameshapoteza michezo 27 na wameshinda michezo 24.
Kwingineko kwenye NBA, Philadelphia 76ers wamerejea kwenye nafasi ya kwanza ya Eastern Conference baada ya kuwafunga Boston Celtics (106-96). LA Lakers wamewagaraza Toronto Raptors kwa pointi 110-101.
INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.
Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.
CHEZA HAPA
warda
Curry anajitahidi sana
Caroline
Curry. Kaza buti
Hopemwaikuka
Pambana