Ule wakati wa kuitizama kwa makini ligi ya kikapu ya NBA unawadia. Ni muda wa kuiangalia michezo ya mtoano (Play-Offs), burudani ipo huku!!
Pande zote mbili za Ligi ya NBA (Eastern na Western Conference) zinaelekea kwenye hatua ya Play-Offs, baadhi ya timu zitafuzu hatua hiyo, zingine zitakua ndio mwisho wao kwa mwaka huu, 2022.
Phoenix Suns wanakua timu ya kwanza kufanikiwa kufuzu hatua ya mtoano. Hii ni baada ya kupata ushindi wa pointi 111-90 dhidi ya Miami Heats. Devin Booker alikua kinara wa Suns kwa kupachika pointi 23 na kuvusha timu hiyo ambayo, msimu uliopita ilipoteza mchezo wa fainali dhidi ya Milwaukee Bucks.

Kule Staple Centre, LA Lakers wameambulia kipigo cha 6 mfululizo baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Houston Rockets. LeBron James alikuepo uwanjani baada ya kukosekana kwenye mchezo uliopita lakini, matokeo ya pointi 139-130 yalitosha kuongeza kidonda kwa Lakers.
Mabingwa watetezi wa NBA, Milwaukee Bucks, wameendeleza ushindi baada ya kuwafunga Atlanta Hawks kwa pointi 124-115. Chicago Bulls wamevunja utumwa wa kupoteza michezo 5 kwa ushindi wa pointi 114-108 dhidi ya Detroit Pistons.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


