Durant Apigwa Faini Ya Dola 50,000 Kwa Lugha Chafu

Nyota wa mpira wa kikapu wa timu ya Brooklyn Nets, Kevin Durant amepigwa faini ya kulipa faini ya dola 50,000 kwa kosa la kutumia lugha ya matusi kwa mwigizaji Michael Rapaport katika mazungumzo binafsi ya mtandaoni.

Siku ya jumatano kuliibuka mzozo mkali mtandaoni kufuatia picha alizivujisha mwigizaji mkongwe Rapaport kuhusu kupokea jumbe za matusi na vitisho kutoka kwa Kevin Durant.

Katika tweet ya hivi karibuni aliyotoa Rapaport inaonesha mazungumzo yaliyogubikwa na matusi na lugha chafu kutoka kwa watu wengi akiwemo nyota huyo wa Nets.

Durant aliibuka na kuomba radhi kwa umma akidai hakumaanisha hivyo na hakujua jamii imemuelewa vibaya kiasi hicho. Akaongezea kwa kudai kwamba yeye na Rapaport hutaniana mara kwa mara, jambo ambalo Rapaport anapinga.

Taarifa rasmi kutoka NBA linasema chama hicho kimempiga faini ya dola 50,000 kama fundisho kwa wote wanaofikiria kufanya vitu vibaya vya aina hiyo. Durant aliwahi kuhusishwa na kutumia akaunti za bandia mtandaoni!

Kevin Durant
Kevin akiwa mchezoni
Durant amekosa kucheza michezo mingi sana ya Nets msimu huu, je kitendo hiki kitamfanya awe mbali zaidi na wachezaji wenzake.

UNAWEZAJE KUKOSA KASINO YA BREAK AWAY LUCKY WILDS INAYOKUPA NAFASI YA USHINDI MURUA.

Break Away Lucky Wilds ni moja ya Sloti pendwa katika kasino za #meridianbet inayokupa mara 11,000X ya dau lako, unayo nafasi ya kuwa milionea unasubiri nini?

CHEZA HAPA

4 Komentara

    Iwe funzo kwa wengine

    Jibu

    Wachezaji wengine watajifunza

    Jibu

    Safii hilo ni funzo tosha

    Jibu

    Safi kabisa hiyo ni fundisho

    Jibu

Acha ujumbe