Hatua yenye burudani kunako Ligi ya NBA huwa ni michezo ya mtoano (play-Offs). Huku ni timu 2 kuchuana mara 7, hakuna kubahatisha! Miami Heats wamefuzu hatua hiyo.
Katika muendelezo wa Eastern na Western Conferences, Heats wamefuzu hatua ya mtoano baada ya kuwafunga Boston Celtics kwa pointi 129-121. Huu ni ushindi wa 10 kati ya michezo 13 waliyocheza Heats kwa siku za karibuni.
Kuwafunga Celtics, kunawapa nafasi Heats kufuzu kwa kushika nafasi 4 kunako msimamo wa Eastern Conference. Sambamba na Heats, LA Lakers ambayo wanamkosa LeBron James kwa michezo 5 sasa, ameibuka kidedea baada ya kuwafunga New York Knicks.
Ushindi wa Lakers, unawapa matumaini ya kufuzu hatua ya Play-Off msimu huu ambao wanaingia kama mabingwa watetezi wa NBA. Ushindi wa pointi 133-104 dhidi ya Knicks, unawaweka Lakers kwenye nafasi ya 7 nyuma ya Dallas Mavericks waliopoteza mchezo dhidi ya Memphis Grizzlies.
Katika mfumo wa kawaida, timu 6 za juu kwenye misimamo ya Eastern na Western Conference zinafuzu moja kwa moja hatua ya mtoano. Timu zinazoshika nafasi ya 7-10, zitachuana kutafuta nafasi 2 zilizosalia kushiriki hatua hiyo.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Magdalena
Safi sana