Kadri NBA Draft inavyokaribia, Golden State Warriors wanaonekana kuwa na mpango mkubwa ambao unaweza kubadilisha mustakabali wa klabu hiyo. Badala ya kutumia chaguo lao la 11 pekee katika raundi ya kwanza, kuna dalili kuwa Warriors wanaweza kutafuta njia ya kupata chaguo la pili na kuondoka na vipaji viwili vikubwa vitakavyosaidia timu kwa sasa na miaka ijayo.

Katika siku za hivi karibuni, Warriors wamefanya majaribio na wachezaji kadhaa wanaovutia akiwemo Yaxel Lendeborg, Morez Johnson Jr. na Chris Cenac Jr. Pia wamehusishwa na nyota wengine kama Cameron Carr wa Baylor na Labaron Philon Jr. wa Alabama. Hii inaonyesha wazi kuwa viongozi wa timu hiyo wanachunguza kwa kina kundi kubwa la vipaji kabla ya kufanya maamuzi muhimu.
Kinachowapa matumaini zaidi ni kwamba wachambuzi wengi wa NBA wanaamini wachezaji hao watapatikana baada ya pick ya 11. Hali hiyo inafungua uwezekano wa Warriors kupata trade down, kupata chaguo zaidi katika raundi ya kwanza na bado kufanikiwa kupata wachezaji wanaowataka.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Miongoni mwa majina yanayovutia zaidi ni Lendeborg, ambaye mashabiki wengi wanamuona kama mchezaji anayefaa kuungana na Golden State mara moja. Hata hivyo, Morez Johnson Jr. na Chris Cenac Jr. pia wamevutia viongozi wa klabu kutokana na uwezo wao wa ulinzi, nguvu za kimwili na nafasi ya kukua kuwa nyota wakubwa katika siku zijazo.

Ikiwa mpango huu utafanikiwa, Warriors wanaweza kuondoka kwenye NBA Draft ya mwaka huu wakiwa na vipaji viwili badala ya kimoja, jambo ambalo lingewapa nguvu mpya katika kipindi ambacho Stephen Curry, Draymond Green na nyota wengine wa kizazi cha sasa wanakaribia mwisho wa safari zao.


