Pambano kali la kuwania taji la dunia la uzito wa juu wa Uingereza kati ya Tyson Fury na Dillian Whyte linatarajiwa kufanyika leo siku ya Jumamosi usiku wa kuamkia Jumapili.
Fury ambaye hajashindwa anaweka taji lake la WBC mezani dhidi ya raia mwenzake, baada ya kumchapa Deontay Wilder katika pambano lao la tatu lililofanyika Las Vegas Oktoba mwaka jana.
Whyte hajapigana tangu aliposhinda dhidi ya Alexander Povetkin katika mechi yao ya marudiano Machi mwaka jana.
Sasa, wapinzani hao wawili wa ndani watakutana London katika pambano kubwa ambalo litakuwa moja kwa moja kwenye media mbalimbali.
Fury alisema “Ninafuraha sana kurejea kupigana tena Wembley Stadium na ninyi mashabiki mmefanya hili litokee.
“Pongezi nyingi ziende kwa timu ya Dillian Whyte, tunaenda kuonyesha burudani inaenda kuwa vita msijali kuhusu hilo.”
Dillian Whyte alipoulizwa kuhusu umuhimu wa uzito wake, alijibu: “Hakuna, mapambano mengine ni tofauti. Kupigana na mtu mkubwa, mtu mzito zaidi kuliko mimi.
“Tuko tayari kwenda vitani, niamini. Sina wasiwasi na jinsi alivyo.”
Bashiri Pambano hili Hapa
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.