Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetangaza rasmi ratiba ya mashindano ya klabu bingwa barani Afrika kwa msimu wa 2026/27, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho. Ratiba hiyo imeweka wazi tarehe za hatua zote kuanzia raundi za awali hadi fainali, hatua ambayo imezifanya klabu mbalimbali kuanza kupanga maandalizi ya msimu mpya wa kimataifa.
Bingwa mtetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Mamelodi Sundowns, anatarajiwa kurejea kutetea taji lake akiwa na lengo la kuweka historia kwa kuwa klabu ya kwanza kutoka Afrika Kusini kutwaa ubingwa huo mara mbili mfululizo. Orlando Pirates pia watashiriki mashindano hayo baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini msimu wa 2025/26, huku Kaizer Chiefs na Durban City wakiiwakilisha nchi hiyo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
CAF imesema kuwa droo ya mashindano hayo bado haijafanyika, lakini kutokana na viwango vya ubora wa vilabu, Sundowns anatarajiwa kupewa nafasi ya kuanzia hatua ya pili ya mchujo bila kucheza raundi ya kwanza. Hali kama hiyo pia inaweza kuikumba Kaizer Chiefs katika Kombe la Shirikisho kutokana na nafasi yake kwenye viwango vya CAF.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, raundi ya kwanza ya mchujo itachezwa kati ya Septemba 4–6 na marudiano Septemba 11–13, huku raundi ya pili ikipangwa kufanyika Oktoba 16–18 na marudiano Oktoba 23–25. Hatua ya makundi itaanza Novemba 27–29 kabla ya kuendelea mwezi Desemba na kukamilika Januari 2027, ambapo timu nane bora kutoka kila mashindano zitafuzu hatua ya robo fainali.
“Robo fainali zitachezwa Februari 26–28 (mkondo wa kwanza) na Machi 5–7, 2027 (marudiano), nusu fainali Aprili 9–11 na Aprili 16–18, huku fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho zikitarajiwa kufanyika kati ya Mei 9 hadi Mei 31, 2027,” imesema CAF katika ratiba yake rasmi, ikieleza kuwa tarehe kamili za fainali zitatangazwa baadaye kutokana na maandalizi ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 zitakazoandaliwa na Tanzania, Kenya na Uganda.


