Rais wa Shirikisho la Soka Afrika, Patrice Motsepe, ametoa ujumbe mzito wa matumaini kwa mataifa ya Afrika kuelekea FIFA World Cup 2026, akisisitiza imani yake kuwa bara hilo lina uwezo wa kufika mbali katika michuano hiyo.
Akizungumza na wanahabari nchini Senegal, Motsepe aliweka wazi matarajio yake makubwa kwa timu za Afrika, hasa akilitaja taifa la Senegal kuwa na nafasi ya kufika hatua ya juu kabisa ya mashindano hayo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Nadhani nitaiona Senegal kwenye fainali ya Kombe la Dunia kule Marekani! Na labda hata mataifa mawili ya Afrika yakikutana fainali,” alisema Patrice Motsepe.
Aliongeza kwa msisitizo wa imani akisema “Inshallah, tukutane fainali? Hilo litaifanya Afrika ijivunie,” kauli ambayo ilipokelewa kwa shangwe na makofi makali kutoka kwa wanahabari waliokuwepo.
Ujumbe huo umeongeza ari kwa mataifa 10 ya Afrika yanayotarajiwa kushiriki Kombe la Dunia 2026, huku ukionekana kuwa kichocheo cha matumaini kwa bara zima katika juhudi za kufanya vizuri zaidi kwenye jukwaa la kimataifa.


