Licha ya uamuzi uliotikisa ulimwengu wa soka uliotolewa na CAF wa kuwapokonya ubingwa wa AFCON 2025, kikosi cha timu ya taifa ya Senegal kimewasili kambini kikiwa na morali ya hali ya juu kuelekea mechi za kirafiki za kimataifa.
Senegal inatarajiwa kucheza dhidi ya Peru national football team Machi 28 nchini Ufaransa, kabla ya kuikaribisha Gambia national football team Machi 31 jijini Dakar.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Uamuzi wa CAF uliotolewa Machi 17, 2026 uliipa ubingwa timu ya taifa ya Morocco baada ya kudai kuwa Senegal ilifanya kitendo cha walk-off wakati wa fainali ya Januari 18, na hivyo matokeo kubadilishwa kuwa ushindi wa mabao 3-0 kwa Morocco.
Hata hivyo, nyota wa Senegal akiwemo Sadio Mané pamoja na Moussa Niakhaté wameonekana wakiwa na furaha kambini, wakisisitiza kuwa wanaamini wao ndio mabingwa halali wa michuano hiyo licha ya maamuzi hayo.
Kwa upande mwingine, Shirikisho la mpila wamiguu Senegal tayari imewasilisha rufaa katika mahakama ya michezo CAS kupinga uamuzi huo, huku mashabiki wengi wa Senegal wakiendelea kuamini kuwa ushindi wao ulipatikana kihalali uwanjani.

