Mabingwa wa Afrika Mamelodi Sundowns wameandika historia kwa kutwaa taji lao la pili la CAF Champions League baada ya kuifunga AS FAR kwa jumla ya mabao 2-1 kufuatia sare ya 1-1 katika mchezo wa marudiano uliochezwa Rabat nchini Morocco.
Ushindi huo umefuta maumivu ya misimu ya nyuma ambapo Sundowns ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri lakini kushindwa kufika mwisho, huku safari ya msimu huu ikithibitisha ubora wao barani Afrika kupitia takwimu mbalimbali za kuvutia.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Sundowns ilimaliza michuano hiyo bila kupoteza mchezo wowote nyumbani, ikishinda mechi sita na kutoka sare moja, huku ikifunga mabao 23 katika michezo 14 na kuruhusu mabao 10 pekee katika kampeni nzima.
“Sundowns ilionyesha uthabiti mkubwa msimu huu, hasa katika michezo ya nyumbani ambapo waliendelea kudumisha rekodi yao bora kwenye michuano hiyo,” ilieleza taarifa hiyo.
Kocha Miguel Cardoso alifanikiwa kutwaa taji hilo katika jaribio lake la tatu baada ya kupoteza fainali mbili zilizopita, huku kiungo mshambuliaji Nuno Santos akiwa mchezaji aliyehusika na mabao mengi zaidi kwa Sundowns baada ya kufunga mabao matatu na kutoa pasi tano za mabao.
“Mchango wa Nuno Santos pamoja na uimara wa safu ya ulinzi chini ya kipa Ronwen Williams ulikuwa muhimu sana kwenye mafanikio ya timu,” iliongeza taarifa hiyo.
Beki wa kulia Khuliso Mudau ndiye aliyekuwa mchezaji wa Sundowns aliyecheza dakika nyingi zaidi kwenye michuano hiyo akiwa na dakika 1,239, huku kinda Kutlwano Lethlaku mwenye miaka 20 akiweka rekodi ya kuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuanza katika fainali ya CAF Champions League kwa upande wa Sundowns.


