Diego Simeone ameipita rekodi ya Luis Aragones ya kushinda mechi nyingi ndani ya Atletico Madrid kama kocha mkuu.
Kocha huyo wa Argentina alifikisha ushindi wa 309 siku ya Jumatano kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Athletic Bilbao matikeo yaliyoipeleka Atletico nafasi ya kwanza kwa tofauti ya lama sita mbele ya Barcelona na Real Madrid katika jedwali la LaLiga.
Iker Munian aliipa Athletic Bilbao goli la kuongoza katik dimba la Wanda Metropolitano,lakini Marcos Rlorente alisawazisha mwishoni mwa kipindi cha kwanza na Luis Suarez alifunga bao la pili kwa mkwaju wa penati mapema kipndi cha pili.
Ushindi wa mwisho wa wa Simeone umepatikana katika mechi yake 514 akiwa kama meneja.Aragones mtu pekee aliyeiongoza Atletico kwenye michezo mingi alifikisha ushindi wa 308 katika mechi 612.
Atletico imeenda sare mara 121 na kupoteza 84 wakiwa chini ya Simeone ambaye alichukua mikoba ya kuinoa timu hiyo mwaka 2011 na anaenda kuwa kocha wao mwenye mafanikio wa muda wote.
Simeone ameshinda mataji saba zaidi ya Aragones ambaye alishinda mataji sita pekee.
warda
Atletico round hii hawashikiki
Venerose
Pongezi kwake Diego
Lydia Emmanuel Magoti
Pongez kwake
Hopemwaikuka
Katishaa
Caroline
Simeone anakuja vizuri
Neema juma
Pongezi kwake
Sarah
Pongezi kwake
Issa
Kocha bora