Cesc Fabregas Ameandika Historia Akiwa na Como 1907: “Sisi si Inter Milan, AC Milan au Juventus FC.”

Cesc Fabregas amesema anajisikia furaha sana na kujivunia baada ya kuipeleka Como 1907 kufuzu michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza kabisa, na akaongeza kuwa timu yake inatarajia kuruka juu zaidi kabla ya mwisho wa msimu wa 2025-26: “Sisi si AC Milan, Inter Milan, Juventus FC au SSC Napoli.”

Cesc Fabregas Ameandika Historia Akiwa na Como 1907: “Sisi si Inter Milan, AC Milan au Juventus FC.”

Como 1907 walipata ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya Hellas Verona FC katika Serie A, bao pekee likifungwa na Tasos Douvikas siku ya Jumapili mchana. Ushindi huo unamaanisha kuwa timu hiyo haiwezi tena kumaliza chini ya nafasi ya sita msimu huu.

Como tayari wamehakikishiwa nafasi katika UEFA Europa Conference League, lakini bado wanaendelea kupigania nafasi za UEFA Europa League na UEFA Champions League kuelekea mechi mbili za mwisho za msimu wa 2025-26.

Leo ni miaka miwili kamili tangu Como 1907 walipopanda daraja kutoka Serie B. Cesc Fàbregas aliiongoza timu hiyo kumaliza katika nusu ya juu ya msimamo kwenye msimu wao wa kwanza kurejea ligi kuu mwaka 2024-25, na sasa ameihakikishia kufuzu michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo.

“Nina furaha sana na ninajivunia leo,” Mhispania huyo aliambia DAZN baada ya mchezo kumalizika mjini Verona.

“Miaka miwili iliyopita siku kama ya leo tulipanda kwenda Serie A na leo tumefuzu Ulaya. Timu, klabu na mashabiki wote wamekua: Haiwezi kuelezeka. Tutakumbuka siku hii hata baada ya miaka ishirini ijayo.

Siku hizi, kutokana na mitandao ya kijamii, kila kitu kinaenda haraka sana, kuna presha kubwa mno. Lazima ufurahie nyakati hizi. Sikumbuki ni mataji mangapi nimeshawahi kushinda, lakini bado kuna mengi yanakuja. Sasa tumebakiza michezo miwili na tutaona kama tunaweza kuruka juu zaidi. Alisema kocha huyo.

Cesc Fabregas Ameandika Historia Akiwa na Como 1907: “Sisi si Inter Milan, AC Milan au Juventus FC.”

Como 1907 walikuwa miongoni mwa klabu tano zilizotumia fedha nyingi zaidi katika dirisha la usajili la kiangazi, na walitumia zaidi ya klabu nyingine yoyote nchini Italy katika dirisha la majira ya baridi la mwaka 2025. Hata hivyo, Cesc Fàbregas bado ameendelea kusifiwa kwa mtindo wa soka alioujenga ndani ya timu hiyo.

“Kuna mechi nyingi sana katika msimu, hatuwezi kucheza kwa mtindo uleule kila wakati,” kocha Cesc Fàbregas alisisitiza. “Mashabiki wengi leo wamenitumia ujumbe wakikumbuka tulipokuwa Serie D. Sisi si AC Milan, Inter Milan, Juventus FC au SSC Napoli, sisi ni timu ya kawaida yenye unyenyekevu na tunataka kufurahia wakati huu.”

Cesc Fàbregas alikuwa amepanga kusafiri kwenda Spain kutazama mechi ya El Clásico kati ya FC Barcelona na Real Madrid CF baadaye jioni hiyo, lakini sherehe za Como zinaweza kumbadilisha mawazo yake: “Nina ndege saa 17:30, sijui kama nitaenda kutazama El Clasico, nitaamua baada ya nusu saa.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.