Golikipa wa Milan, Gianluigi Donnarumma amefikisha idadi ya kucheza mechi 200 za Serie A na yupo kwenye mchakato wa kuvunja rekodi hiyo.
Donnarumma alifikisha karne mbili wakati wa mchezo wa derby dhidi ya Inter siku ya Jumapili.
Katika miaka 21 na siku 361, mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia ndiye mchanga zaidi kufanikiwa katika mashindano hayo tangu mwaka 1994-95.
Mkongwe Gianluigi Buffon hapo awali aliweka rekodi hiyo akiwa na (miaka 24 na siku 83).
Donnarumma alipewa mchezo wake wa kwanza wa ligi akiwa na miaka 16 na bosi wa Milan wa wakati huo Sinisa Mihajlovic, Oktoba 2015. Ameokoa asilimia 73.09 ya mashuti wakati wa taaluma yake katika ligi kuu ya Italia, na pia kuokoa penati nane.
Ikilinganishwa na makipa wengine ambao wamecheza angalau michezo 10 ya Serie A msimu huu, ni Lukasz Skorupski tu (73.26) wa Bologna na Mattia Perin wa Genoa (72.41) ndiye anayeweza kuokoa asilimia ya Donnarumma ya amabye anawastani wa 72.15.
Mechi ya 174 ya Milan Debi huko Serie A ilishuhudia wapinzani wakiingia kwenye mechi hiyo wakishika nafasi mbili za juu kwenye msimamo kwa mara ya kwanza tangu Aprili 2011. Rossoneri ilishinda 3-0 kwenye hafla hiyo na ikaenda kumaliza msimu kama mabingwa.
Treasure Heroes inakupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!
warda
Hongera yake
Hopemwaikuka
Saf sana
Venerose
Aendelee kuongeza bidii ili afike mbali zaid
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Issa
Kipa bora seria a
Neema juma
Asibwetekee aongeze juhudi