Fowadi wa Barcelona Antoine Griezmann alimtaja Lionel Messi kama “Legend” baada ya nahodha huyo mashuhuri kutawala vichwa vya habari siku ya Jumapili.
Messi alianza kufunga kwa mpira wa adhabu dakika ya 20 na lilikuwa bao lake la 650 kwa Barca – kabla ya bao la Jordi Alba la kujifunga na kufanya ubao usomeke 1-1, ingawa Griezmann alifunga goli la pili na la ushindi kwa Barca dhidi ya Athletic Bilabao dakika 16 kabla ya kipyenga cha mwisho.
Baada ya gazeti la El Mundo kudai mkataba ambao Messi alisaini Camp Nou mwaka 2017 – ambao unamalizika mwishoni mwa msimu – una thamani ya zaidi ya milioni 555, Griezmann aliulizwa juu ya thamani ya mtu huyo wa miaka 33.
“Tunafurahi na Messi, ni legend (gwiji),” Griezmann alimwambia Movistar.
“Tunatumahi tunaweza kuendelea kufurahiya naye na anaweza kuendelea kutusaidia kushinda.”
Messi – anayetajwa kuondoka Barca huku akiwa na uhusiano mzuri na Paris Saint-Germain na Manchester City – amefunga mabao mawili ya moja kwa moja kutoka kwa majaribio yake manne ya mwisho kwa Barcelona kwenye mashindano yote, baada ya kufunga moja tu kutoka kwa majaribio 62 ya awali.
Kati ya mabao 650 ya Messi kwa Barcelona, 49 kati yao yamekuwa ni ya free-kick na 38 kati ya hayo amefunga katika LaLiga.
Messi ana mabao 12 na assist mbili kwenye ligi hiyo kwa Barca, ambao wako nafasi ya pili na alama 10 nyuma ya viongozi Atletico Madrid.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.
Sania
Messi baba lao
Neema juma
Ni kweli kabisaa messi lazima apewe sifa
Rahma
Messi asaivi analudi kivingine
Magdalena
Messi ni balaaa
Dorophina
Griezmann yupo sahihi Messi jembe
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Messi mtu mbaya
Caroline
Messi ni legend kweli kabisa
Hopemwaikuka
Anastahir pongez
samiah
gud
Janeflora malisa
Safi
warda
Mie kwangu ni CR7