Pep Guardiola amelezea furaha yake baada ya Manchester City kuweka historia kwa kufunga Swansea City bao 3-1 na kusonga mpaka hatua ya robo fainali ya FA Cup.
Mabingwa na viongozi wa Premier League waliifunga timu ya Championship katika dimba la Liberty Stadium na kukamilisha idadi ya kushinda mechi 15 mfululizo na kuweka rekodi kwa hiyo katika timu hiyo ya EPL.
Kyle Walker alifunga goli la ufunguzi katika kipindi cha kwanza kabla ya Raheem Sterling kufunga goli lake la 12 kwa msimu huu mapema mwa kipindi cha pili na goli la tatu liliwekwa kimiani na Gabriel Jesus dakika chache baadaye.
Morgan Whittaker alifunga goli la kufutia machozi kwa upande wa Swansea City baada ya kupata kiungo wa Hispania Rodri kutolewa nje kwa majerha ambayo Guardiola amesema siyo kubwa sana.
Aliulizwa kuhusu rekodi mpya aliyoweka bosi huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich alisema: ” Huu ni ujumbe kwetu sisi wenyewe, tulikuja kushinda hicho ndiyo kitu cha umuhimu.
“Hatuwezi kukataa jinsi tunavyojisikia na kujivunia tulikuwa tunahitaji kuvunja rekodi hii kwa muda mrefu rekodi zipo kwaajili ya kuvunjwa.
“Siyo rahisi kwa soka la kisasa kushinda katika michezo 15 mfululizo tunajivunia na kufurahia na klabu yetu.
Guardiola atakuwa na tumaini la kuongeza point katika Premier League siku ya Jumamosi pale watakapo kabiliana na Tottenham katika dimba la Etihad Stadium.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Sadick
Guardiola ndiye kocha bora duniani kwa sasa. Ni rekodi inayovutia sana
Caroline
Hongera sana
Magdalena
Nachompendea guardiola hanaga papara
Lydia Emmanuel Magoti
Hongera yao
Dorophina
Guardiola anajua kuiongoza sana klabu ya man city ndie kocha bora zaidi vilabu vyote
Samira
Guadiola ni kocha mzuri sana
Khadija
Hongera sana
Issa
Pep mida yake ya kutawala
Angelina
Pep yuko vizur
Sania
Pep yupo makini
Mwanahamisi
Hongera sana
Neema juma
Hongera sana
Hopemwaikuka
Namkubal
warda
Amerudi kwa kishindo