Nyota wa Real Madrid Eden Hazard amesema kwamba anataka kuendelea kucheza kwa muda usiopungua miaka mitano mingine kati ya sita na mshambuliaji huyo alisisitiza kwamba kupata majeraha siyo mwisho wa dunia hali yakuwa amekuwa na changamoto ya kuwa fit huko Bernabeu.
Hazard aliondoka Chelsea na kutua Madrid kwa dau la €100m mwaka 2019 lakini tangu aanze kucheza ndani ya Uhispania amekuwa akikabiliwa na tatizo la majeraha ya mara kwa mara.
Mchezaji huyo wa miaka 30 ambaye anajiandaa kukosa ” wiki mbili au tau” kutokana na kupata tatizo la misuli katika mguu wake wa kushoto, ameanza katika michezo 20 katika LaLiga sita kati ya hiyo ilikuwa ni ya msimu huuna amefanikiwa kufunga mabao matatu pekee.
Hazard ameshindwa kumaliza dakika zote 90 kwenye mchezo wowote wa Madrid msimu 2020-21 katika mashindano yote, lakini Mbeligiji huyo bado ana mawazo chanya juu ya kinachoendelea katika soka lake.
“Bado ninatumaini la kucheza kwa muda mrefu kadri nitavyokuwa sawa na nimekuwa nikijaribu kujifurahisha mimi mwenyewe ndani ya uwanja,” aliiambia On The Front Foot.
“Linapokuja suala la kumaliza soka langu naweza kuangalia nyuma mafanikio niliyopata, lakini kipaumbele chnagu sasa ni kucheza vizuri na kufurahia mpira wa miguu.
“Nimefikisha miaka 30 sasa kama mwili wangu utakuwa sawa nitumaini langu naweza kuendelea kucheza kwa kipindi kisicho pungua miaka mitano au sita.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.
Dorophina
Hazard yupo sahihi bado yupo fiti kuendelea kutumikia klabu yake kwa miaka mitano mingine
Magdalena
Kama bado yupo na nguvu anaweza akaendelea tu
Venerose
Kama uwezo anao aendelee tu
Mwanahamisi
Hazard yupo sahihi
Sarah
Kama bado Yuko vizuri aendelee
Angelina
Nice update
Ernest Kimeru
Pancha ya Hazard inamnyima raha sana
Lydia Emmanuel Magoti
Hazard yupo vizuri
Caroline
Good news
Sadick
Mchango wako Chelsea hautasahaulika, lakini mambo yamekuwa magumu mno kwa tangua atue Real Madrid
Hopemwaikuka
Uwezo unaruhusu
Rahma
Nice
Sania
Hazard aendelee kujituma tu
warda
Ataweza kweli