Kocha wa Inter Miami Phil Neville amekataa hatua ya kutaka kumleta mshindi wa Kombe la Dunia Lionel Messi kwenye Ligi Kuu ya Marekani MLS. Ukiwa na meridianbet unaweza kubashiri mubashara, tembelea maduka ya meridianbet uweze kubashiri.
Miami na Messi walionekana kukaribia makubaliano mwaka jana kama ilivyoripotiwa na Sportsmail mnamo Novemba 27, lakini gwiji huyo wa Argentina sasa anafikiriwa kupendelea kuongeza muda wake mjini Paris baada ya kufanya vizuri kwenye Kombe la Dunia nchini Qatar.
Mkataba wake wa sasa na Paris Saint-Germain unamalizika mwishoni mwa msimu. Beti na Meridianbet mechi za ligi zote, Odds ni kubwa sana, Usikose hii!!.
Akizungumza Jumatatu wakati timu yake ikirejea kwenye mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya, kocha Neville aliulizwa ikiwa kweli uhamisho wa Messi unaweza kutimia.
“Tunataka kuleta wachezaji bora zaidi duniani kwenye klabu hii na pengine ndiye mchezaji bora, hivyo kwetu sisi mazingira hayajabadilika hata kidogo,” Neville alisema.
“Kwa makubaliano yoyote kwa DP yoyote (Mchezaji Mteule) wa kiwango hicho, ni ngumu. Inachukua muda.”
Neville alikabiliana na vyombo vya habari pamoja na nahodha wa Miami Gregore, ambaye pia hakufanya lolote kupunguza hamu ya Messi.
“Kwa nini isiwe hivyo? Ninaamini inaweza kutokea,” alisema. ‘Wachezaji kote ulimwenguni wanaona MLS kama ligi kuu.
“Kama Messi atakuja, ningefurahi kwa sababu napenda kucheza na walio bora na kujifunza kutoka kwao.”
Messi, 35, analipwa karibu $1.45million kwa wiki nchini Ufaransa na angehitaji kupunguzwa mshahara ili kujiunga na timu inayomilikiwa na David Beckham. Na wewe Odds kubwa za soka uanzipata Meridianbet.
Bado angetarajia kuwa mchezaji wa soka anayelipwa zaidi Marekani, na hatua hiyo itakuwa nafasi kubwa kwa Messi kutengeneza zaidi chapa yake.
Miami inaelekea msimu wa 2023 ikihitaji mshambuliaji mpya baada ya Gonzalo Higuain kustaafu mwishoni mwa kampeni ya 2022.
Inaonekana dili linaweza kukaribia kwa mshambuliaji wa Atlanta United Josef Martinez – Neville alimsifu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29.
“Ninampenda daima amefunga mabao dhidi yetu,” Neville alisema. ‘Kuna wachezaji fulani ambao wanavutia sana kiwango cha uwanja, na Josef ni mmoja.
“Yeye ni mashine, ana njaa, anafunga mabao na hahitaji nafasi nyingi. Tuna hatua za kuvutia za kufanya lakini ninakipenda kikosi tulichonacho hivi sasa.’
Miami, ambayo ilifanya mchujo mwaka jana, inaanza msimu wake Februari 25 dhidi ya Montreal.
Wakati huo huo, Messi amerejea mazoezini na PSG baada ya Argentina kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia. Pata Odds kubwa za soka ukiwa na Meridianbet.