Barcelona watalazimika kulipa kiasi cha £46.7m ili kuweza kumnasa mshambuliaji wa Manchester City Ferran Torres na nyongeza ya kiasi cha £8.5m.

City hawajalipa nyongeza yoyote iliyokubaliwa kwa Valencia kutokana na muda mfupi ambao ametumia Etihad.
Barcelona inamchukulia Torres kama moja ya vipaji vya Uhispania na wana pesa za kutumia kwenye dirisha la Januari baada ya kupokea uwekezaji mkubwa hivi karibuni kutoka mkopo wa benki.
Ferran Torres mwenye umri wa miaka 21 ameichezea City michezo minne pekee msimu huu akifanikiwa kufunga mara mbili na bao moja kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa
Barcelona pia imeonyesha kuvutiwa na kumsajili Raheem Sterling lakini kwa sasa Man City wamebadili mawazo yao na wanataka kumbakisha huko Etihad sababu hivi karibuni amerejea kwenye kiwango chake bora.
Kwa sasa Torres yupo nje ya dimba kutokana jeraha la mguu tangu mwezi Oktoba alipoumia akiwa kwenye majukumu na timu ya taifa.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


