Manchester United Kutaka Saini ya Kane

Uongozi wa Manchester United unapiga mahesabu ya kuipata saini ya kiungo nyota wa timu ya Tottenham Hotspurs, Harry Kane kwa ajili ya kujiunga na kikosi hicho msimu ujao.

Ripoti zinasema Manchester United wana matumaini makubwa ya kuipata saini ya mshambuliaji huyo wa Tottenham, Harry Kane mwenye uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu

Manchester United Harry kane
Kocha wa Manchester United Ole ankinong’ona na Mshambululiaji wa Tottenham, Harry Kane uwanjani.

Imeelezwa uongozi wa Timu ya Manchester umeweka dau la Euro Millioni 90 mezani kwa ajili ya kupata saini ya mshambuliaji huyo.

Mpango huo ulikuwepo kwa muda mrefu ila huenda ukakamilishwa kwa haraka kutokana na presha ambayo wanaipata kutoka kwa mashabiki ambao waliandama Jumapili ndani ya Uwanja wa Old Trafford jambo lililofanya mchezo wa United dhidi ya Liverpool upelekwe mbele.

Manchester United fans
Mashabiki wa Manchester United wakiandamana katika Uwanja wa nyumbani wa timu hio, Old Trafford.

Mashabiki wa Manchester United wamesema ya kuwa hawana imani na Joel na Avram Glazer kutokana na uongozi wa kutokuwa na uwazi pamoja na kushindwa kupata mataji. Jambo linalosababisha hasara kwao pamoja na suala la wao kujiunga na European Super League.


TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO

Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!

SOMA ZAIDI

8 Komentara

    Safi sana wakaze buti

    Jibu

    Wangemchukua tu Kane

    Jibu

    Kane wakimpata itakua pouwah sana

    Jibu

    Hapo ni Hela tu mnaweza kumpata mshambuliaji huyo

    Jibu

    Kane yupo vizuri wamchukuwe

    Jibu

    Watakuwa wamepata bonge la mchezaji

    Jibu

    Safii sana

    Jibu

Acha ujumbe