Uongozi wa Manchester United unapiga mahesabu ya kuipata saini ya kiungo nyota wa timu ya Tottenham Hotspurs, Harry Kane kwa ajili ya kujiunga na kikosi hicho msimu ujao.
Ripoti zinasema Manchester United wana matumaini makubwa ya kuipata saini ya mshambuliaji huyo wa Tottenham, Harry Kane mwenye uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu
Imeelezwa uongozi wa Timu ya Manchester umeweka dau la Euro Millioni 90 mezani kwa ajili ya kupata saini ya mshambuliaji huyo.
Mpango huo ulikuwepo kwa muda mrefu ila huenda ukakamilishwa kwa haraka kutokana na presha ambayo wanaipata kutoka kwa mashabiki ambao waliandama Jumapili ndani ya Uwanja wa Old Trafford jambo lililofanya mchezo wa United dhidi ya Liverpool upelekwe mbele.
Mashabiki wa Manchester United wamesema ya kuwa hawana imani na Joel na Avram Glazer kutokana na uongozi wa kutokuwa na uwazi pamoja na kushindwa kupata mataji. Jambo linalosababisha hasara kwao pamoja na suala la wao kujiunga na European Super League.
TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO
Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!
Elika
Safi sana wakaze buti
Venerose
Wangemchukua tu Kane
aisha
Kane wakimpata itakua pouwah sana
[email protected]
Wamchukue tu uyo kane
Johnmary jo
Hapo ni Hela tu mnaweza kumpata mshambuliaji huyo
Adelta
Kane yupo vizuri wamchukuwe
Sauda
Watakuwa wamepata bonge la mchezaji
Lydia Emmanuel Magoti
Safii sana