Mkataba wa Kylian Mbappe unatarajia kuisha mwaka ujao majira ya joto na Mfaransa huyo amesema kwamba bado hana uhakika kama Paris Saint-Germain ni sehemu bora kwake.
Mchezaji huyo wa ufaransa ni moja ya wachezaji bora na akiwa na umri wa miaka 22 tu tayari ameonekana kuwa ni bidhaa inayohitajika na vilabu kama Real Madrid.
Akiongea na France Football, Mbappe alisema kwamba anafuraha huko PSG, lakini alikiri kwamba hana uhakika kama ni sehemu bora katika soka lake.
“Napaswa kufanya maamuzi sahihi na ni ngumu… na ni lazima nitoe kila fursa kufanya maamuzi mazuri,” aliiambia France Football.
“Nipo katika sehemu ambayo nina ipenda, ambapo ninajiskia vizuri, lakini sehemu bora kwangu? Bado sina majibu.
Kama Mbappe ataamua kuondoka PSG, atafanya uso kwa uso na bila kuisaliti timu yake.
“PSG inaelewa ombi langu kwa sababu wanajua kwamba siendi kufanya ualimu wowote wa kuondoka,” alisema.
Kuwa mchezaji mkubwa pia ni kujua namna ya kufanya mambo kwa njia safi na bora nke ya uwanja.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.
Mbappe angeenda ambapo ni sahihi kwake
Asante kwa taarifa