Jose Mourinho anamtaka Harry Kane kucheza ‘kila dakika ya kila mechi” lakini amesema kwamba kinara wa mabao wa Tottenham alitakiwa kupumzika siku ya Alhamisi kwaajili ya kujitazamia hali yake ya kiafya.
Kane alipata tatizo la kifundo cha mguu kwenye mechi ya kupoteza kwa Liverpool mwezi Januari 28 na anaonekana anaweza kukosa wiki kadhaa alirejea dimbani kwenye mchezo dhidi ya West Brom Februari 7.
Ilikuwa ni hatua ambayo iliwapa Spurs ushindi wa 2-0 na ulikuwa ushindi pekee ambao walipata katika michezo mitano iliyopita.
Baada ya kupoteza kwa Everton katika michuano ya FA Cup na kucheza dhidi ya Manchester City wiki iliyopita Kane hakuweza kusafiri mpaka Budapest kwa mchezo wa kwanza wa Europa League dhidi ya Wolfsberger siku ya Alhamisi
Tottenham walifanya kazi yao bila nyota wao Kane, na Son Heung-min, Gareth Bale, Lucas Moura na Carlos Vinicius walifunga mabao manne katika ushindi wa 4-1 wakiwa na faaida ya mabao manne ugenini.
“Anajua kwamba namtaka kucheza kila dakika ya kila mechi kwa hiyo sio swala kuchagua,” Mourinho aliongea na waandishi alipoulizwa kuhusu Kane.
Kane amekuwa mfungaji bora msimu huu akiwa na Son akiwa ameweka kambani mabao 13 wakati pia nahodha huyo wa Uingereza ametoa asisti 11.
Treasure Heroes inakupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!
Adelta
Kane ni mchezaji makini
Neema juma
Yuko vizuri ndio maana anamuhitaji
Hopemwaikuka
Am happy for him
Caroline
Kane ni mchezaj mzuri
Dorophina
Pole yake kane Mourinho ameongea sahihi klabu yake inamuhitaji sana kane
Rahma
Ni mchezaji mzuri sana na ndomana wanamuitaji
Angelina
Nice update
Lydia Emmanuel Magoti
Kane yupo vizuri
Mwanahamisi
Nice
warda
Mourinho akikupenda kakupenda