Harry Kane alitolewa wakati wa mchezo dhidi ya Dinamo Zagreb katika michuano ya Europa League baada ya kupata tatizo la goti lakiwa atakuwa fit kwaajili ya kuwakabili Arsenal siku ya Jumapili hii ni kwa mujibu wa kocha mkuu wa Tottenham Jose Mourinho.
Staa wa Spurs Kane alifunga mabao yote mawili katika ushindi wa 2-0 siku ya Alhamisi katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora katika dimba la Tottenham Stadium.
Mourinho alimtoa Kane wakati pia mchezaji Tanguy Ndombele alitolewa mapema baada ya bao la pili kufungwa.
Lakini Mourinho anajiamini wawili hao wote watapatikana na kuwa tayari kwaajili ya debi ya Londoni wikendi hii.
Aliulizwa kama kuna jambo lolote la kuongea kuhusu Ndombele, Mourinho aliiambia BT Sport: “Sidhani kama ninalo, hata kwa Harry, siamini kama kuna jambo lolote kubwa.
“Ujue kuna mechi ambayo kila mtu anataka kucheza na vitu vidpgo haviwezi kwenda kuwazuia kucheza siku ya Jumapili, naamini watakuwa vizuri.
Kane ambaye alikuwa na mashuti matatu na kutengeneza nafasi mbili kwenye mechi ya jana, sasa amehusika kwenye mabao sita (amefunga mara nne na kutoa asisti mbili) katika mechi mbili za Spurs zilizopita.
Angelina
Bonge la game
Rahma
Asante kwa taalifa
Hopemwaikuka
Habar nzur hii
Venerose
Asante kwa makala
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri game lakufa mtu hilo
Caroline
Good
warda
Litakuwa bonge la mechi