Kocha mkuu wa Bayern Munich Julian Nagelsmann amesema kwamba aliwasiliana na Joshua Kimmich baada ya kiungo huyo wa Ujerumani kukiri kwamba hajapata chanjo ya COVID-19.

Bayern Munich ambao wanajiandaa kucheza dhidi ya Borussia Monchengladbach katika michuano ya DFB-Pokal ikiwa ni hatua ya pili wamekuwa bila kocha wao baada ya kocha huyo wa zamani wa RB Leipzig kugundulika kuwa na maambukizi ya coronavirus.
Kimmich ambaye alikuwa mchezaji muhimu katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Hoffenheim alielezea kwamba haja chanja kwa sababu anataka kufanya uchunguzi zaidi kabla ya kujihusisha na mpango huo.

Rais wa zamani wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge haraka alijibu kwamba Kimmich anapaswa kupata chanjo ingawa Nagelsmann aliingilia kati kumaliza sakata siku ya Jumanne.
” Kuna mambo mengi yakuongelea,” Nagelsmann aliwaambia maripota akiwa nyumabani akihojiwa kwa video. “Ni muhimu kila mtu kuwa na maoni yake na kuamua wenyewe kwenye kila jambo.
“Nilimwandikia ujumbe baada ya mahojiano yale nilimwambia kwamba kuna maswala rahisi sana ya kuongelea ukiwa kwenye jumuiya.
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA


