Pep Guardiola anasema hakuridhishwa na Riyad Mahrez kwa kupuuzia maelekezo yake katika kipindi cha kwanza katika ushindi wa 6-3 dhidi ya RB Leipzig katika mchezo wa ligi ya mabingwa usiku wa jumatano.
Mkufunzi huyo kutoka Hispania anaingia kwenye kumbukumbu za kushindaΒ michezo 87 katika mashindano ya Ulaya huku akimtoa Arsene Wenger katika nafasi ya tatu.
Guardiola japo alikuwa anaongoza mpaka dakika ya 63 kwa 4-2 lakini hakufurahishwa na kiwango cha Mahrez na kumwita kumfokea. Grealish pia alikumbana na hasira za Guardiola, mkufunzi huyo hakufurahishwa na kasi ya ushambuliaji wake.
Ushindi wa goli sita haukumfanya Guardiola kutulia na alipoulizwa kwa nini aliwafokae wachezaji wake Mahrez na Grealish alisema “tulizungumza jinsi tutakavyocheza lakini hawakufanya kama tulivyo kubaliana.”
Magoli ya Manchester City yalifungwa na Nathan Ake, Jack Grealish, Joao Cancelo, Gabriel Jesus na MahrezΒ huku magori ya Leipzig yakifungwa na Christopher Nkunku aliyefunga goli zote tatu.
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!