Ronaldo Kuongeza Nguvu Kikosi cha United vs Tottenham

Kocha wa muda wa Manchester United Ralf Rangnick amethibitisha mshambuliaji Christiano Ronaldo alirejea mazoezini na anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachomenyana na Tottenham leo katika uwanja wa Old Trafford.

Ronaldo Kuongeza Nguvu Kikosi cha United vs Tottenham

Ronaldo alikosa mchezo wa kupoteza kwa 4-1 dhidi ya City ambao ni mahasimu wao wa jiji la Manchester na ilisemekana kwamba alikuwa akisumbuliwa na jeraha hali iliyopelekea kusafiri mpaka Ureno lakini taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zilidai ni kutoelewana kwa nyota huyo na kocha.

“Alirejea tena mazoezi jana,” Rangnick alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi siku ya Ijumaa.

“Alifanya mazoezi katika kipindi chote cha mazoezi na ninatarajia afanye mazoezi leo pia.

“Alifanya mazoezi vizuri, kama kundi lingine. Ningefikiri angepatikana kesho.”

Ronaldo amefanikiwa kufunga bao 1 pekee bila asisti kwenye michezo 10 msimu huu kwenye mashindano yote. Leo atamaliza ukame wake dhidi ya timu ya Conte?


VUNA MKWANJA NA SHINDANO LA EVOPLAY SPRING AWEKING

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

 

Acha ujumbe