Inawezekana ukawa unajiuliza ni mchezaji gani kutoka Afrika anaongoza kwa magoli mengi katika Premier League kwa sasa? Jibu ni Mohammed Salah mchezaji wa kimataifa wa Misri anayeichezea Liverpool kwa sasa.
Hat-trick ya Salah katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Manchester United ilifanya winga huyo kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika mwenye idadi kubwa mabao kunako Premier League kwa kumpita mkongwe wa Chelsea Didier Drogba mbali na kuweka rekodi mpya pia amekuwa mchezaji wa kwanza wa Kiafrika kufunga hat-trick katika dimba la Old Trafford.
Nyota wa zamani wa Chelsea sasa anashika nafasi ya pili ya wachezaji wa Afrika wenye mabao mengi EPL akiwa na magoli 104 katika mechi 254 nyuma ya Salah aliyefikisha mabao 107 katika michezo 167.
Orodha ya wachezaji 10 wa Afrika wenye magoli mengi EPL.
Mohamed Salah (Chelsea, Liverpool)
- Magoli: 107
- Mechi: 167
Didier Drogba (Chelsea)
- Magoli: 104
- Mechi: 254
Sadio Mane (Southampton, Liverpool)
- Magoli: 100
- Mechi: 238
Emmanuel Adebayor (Arsenal. Man City, Tottenham, Crystal Palace)
- Magoli: 97
- Mechi: 242
Yakubu Ayegbeni (Portsmouth, Middlesbrough, Everton, Blackburn)
- Magoli: 95
- Mechi: 252
Riyad Mahrez (Leicester City, Man City)
- Magoli: 68
- Mechi: 233
Pierre-Emerick Aubameyang (Arsenal)
- Magoli: 68
- Mechi 122
Yaya Toure (Man City)
- Magoli: 62
- Mechi: 230
Nwankwo Kanu (Arsenal, West Brom, Portsmouth)
- Magoli: 54
- Mechi: 273
Efan Ekoku (Norwich, Wimbledon)
- Magoli: 52
- Mechi: 160
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.
CHEZA HAPA