Baada ya kutosikika kwenye masikio ya wapenda soka kwa muda kidogo, hatimaye Bale na Ronaldo wamerejea katika nafasi zao kwa kuzifumania nyavu wikiendi hii.
Gareth Bale alikuwa kwenye kifungo huru ndani ya kikosi cha Real Madrid kabla ya kupata nafasi ya kusajiliwa Tottenham. Hii ilimfanya ateke vichwa vya habari kila kona ya ulimwengu na wapenzi wa soka kupata nafasi ya kumuona tena uwanjani.
Japo alikaa nje kwa muda kidogo, hatimaye alirejea uwanjani na wikiendi hii amepachika goli katika mchezo dhidi ya Brighton Albion na kuisaidia Tottenham kuibuka na ushindi wa magoli 2-1.
Kwingineko kwenye ulimwengu wa soka, tuitizame Ligi ya Italia – Serie A. Siku kadhaa zilizopita, Cristiano Ronaldo aliripotiwa kupata maambukizi ya COVID19 na hivyo alizikosa mechi kadhaa za Serie A pamoja na kipigo kutoka kwa Barcelona kwenye Ligi ya Mabingwa.
Ronaldo alirejea uwanjani wikiendi hii katika mchezo dhidi ya Spezia. Akicheza akitokea benchi, Ronaldo alipachika magoli mawili katika ushindi wa 4-1 kwa miamba ya soka la Italia – Juventus.
Kuimarika kwa kiwango cha Bale ndani ya kikosi cha Tottenham huenda kukaisaidia timu hiyo kufanya vizuri msimu huu. Upande wa pili, kurejea kwa Ronaldo ni habari njema kwa Pirlo kwani shujaa wake ataendelea kuisaidia timu hiyo kupata matokeo hasa kwenye Ligi ya Mabingwa.
Hii ni halisi kwa ajili ya mashujaa wote! Ukiwa jasiri unavuna mkwanja kibao hapa na sloti hii ya Huangdi Casino. Waka nusu tukupe maradufu!
warda
Safi sana Wote Nawakubali
zeiyana
bale bado hanaonesha maajadu yake
Salma ngende
Wako vizuri
Adelta
Bale aongeze juhudi ili aweze kufanya maajabu yake
Dorophina
Habari njema kwa vilabu hivyo viwili
Fatina mfigi
Safi San hiy Ni habar nzur
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Khadija
Safi sana tumefurahi sana mashabiki kusikia mmerudi tena uwanjani
Ester jackson
Safii sana tunaona sasa matunda ya bale pale real Madrid walikuwq wanampotezea mafanikio yake tu .Ronald tulijua tu huyo mzee wakazi anahasira na nyavu no muda wake sasa kuziona Mara kwa Mara kuiwekea timu yake nafasi nzuri
Tatu
Bale na ronaldo naona walipania huo mchezo tuone mechi zijazo kama watafanya vizuri
Elika
Wote wako vizur
Mwajumah
Nawakubali sana hawa jamaa Safi sana
Hopemwaikuka
Hawa watu ni balaa
aisha
Wako vizuri sana
Issa
Miamba hii
Sabrina
Vijana wako vizuri kama bale inaelekea alikua na habu na nyavu madrid walimuweka sana bench
Povel
Cr7 na bale hits in town
Saupha Mohamed
Safii sana
Sauda
Wote wakali
Nasra
Wote wapo vzuri
Fatuma kasomo
Safi sana
Shani
Wantisha san