Uchambuzi EPL: West Ham United vs Manchester City

Manchester City wanania ya kutetea taji la Premier League msimu huu na leo watakuwa na kibarua kigumu mbele ya West Ham United ambao wanataka kucheza tena michuano ya Europa League msimu ujao baada ya kufanya vizuri vyema msimu huu na kutolewa katika nusu ya fainali.

City wamekuwa wakitoa dozi nzito nzito tangu watolewe na Real Madrid katika nusu fainali ya Champions League. Walianza kwa kuibamizia 5-0 Newcastle wakaja kutoa kichapo kingine cha 5-1 kwa Wolves.

Taarifa ya Timu

John Stones, Ruben Dias na Kyle Walker wote hawatocheza sababu ya majeraha huku Aymeric Laporte na Fernandinho pia wakiwa kwenye shaka kumaanisha kwamba Nathan Ake ndiye beki wa kati pekee ndiye ambaye hana tatizo.

Kwa upande West Ham, Michail Antonio na Craig Dawson wote wanatarajiwa kucheza licha ya kutokuwa fit kikamilifu wakati Said Benrahma yupo kwenye shaka kubwa kutokana na jeraha la kifundo cha mguu na Angelo Ogbonna yuko nje kwa mechi zote zilizo salia msimu huu.

Kikosi cha West Ham kinachoweza kuanza: Fabianski; Coufal, Dawson, Zouma, Cresswell; Rice, Soucek; Bowen, Lanzini, Fornals; Antonio

Kikosi cha Manchester City Kinachoweza kuanza: Ederson; Cancelo, Rodri, Ake, Zinchenko; Silva, Gundogan, De Bruyne; Mahrez, Jesus, Sterling


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe