Kocha wa zamani wa Manchester City, Pep Guardiola, ameaga rasmi klabu hiyo huku maelfu ya mashabiki wakijitokeza kushiriki gwaride la ubingwa lililogubikwa na hisia za huzuni na shukrani baada ya miaka 10 ya mafanikio makubwa chini yake.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Mashabiki walijaza mitaa ya Manchester wakishuhudia makombe ya League Cup na FA Cup yakibebwa kwenye mabasi ya wazi, lakini Guardiola ndiye aliyepata shangwe kubwa zaidi. Wengi walieleza maumivu yao kutokana na kuondoka kwake, wakisema ameibadilisha Manchester City na soka la England kwa ujumla.
Wachezaji wa City pia walimpongeza Guardiola pamoja na nyota wanaoondoka klabuni hapo akiwemo Bernardo Silva na John Stones, huku Erling Haaland akisema ni fahari kucheza pamoja nao ndani ya kikosi hicho.
Akizungumza mbele ya mashabiki, Guardiola alisema ataendelea kuikumbuka Manchester City maisha yake yote kutokana na upendo mkubwa alioupata kutoka kwa klabu na mashabiki wake.


