Muendesha magali ya Langalanga Lewis Hamilton anaamini kwa sasa kila muda atakaopta wikiendi ni muda wa kuikomboa timu yake ya Mercedes ambayo imeshindwa mara mbili kwenye mbio za kutafuta nafasi siku ya ijumaa Imola.
Hamilton alishindwa kufanya vizuri kwenye mbio za kutafuta nafasi katika mashindano ya Romagna Grand Prix kwa sekunde elfu nne na pia alishindwa hata kuwepo kwenye kumi bora za mbio hizo, bali alishika nafasi 13 nafasi mbili nyuma dareva mwenzie wa Mercedes George Russell.

“Haukuwa wakati mzuri, kiasiri inavunja moyo, unakuwa na matumaini na unafahamu kuwa kila mmoja nafanya kazi kwa juhudi kiwandani, na vitu havikavia pamoja. Alisema Hamilton.
“Inakatisha tamaa, nadhani tulikuwa chini ya kiwango kama timu leo. Kuna vitu inabidi tuweke sawa ambavyo hatukuvifanya.
‘Bila shaka, tutafanya kazi kwa juhudi tuwezavyo ili kuweza kupata nafasi za juu kwemye mbio za kesho. Zitakuwa mbio ngumu , lakini tunaimani kesho kutakuwa na hali ya hewa nzuri, nani anayejua , huenda tukashika nafasi za juu.”
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.