Habari mbaya kwa wapenzi wa mbio za magari ya Formula 1 (F1), bingwa wa dunia – Lewis Hamilton amekutwa na maambukizi ya COVID19 na atakosa mbio za Sakhir GP wikiendi hii.
Taarifa hii imeripotiwa baada ya timu ya Mercedes kuripoti kuwa Lewis Hamilton alianza kuonesha dalili za mgonjwa wa COVID19 na baada ya kufanyiwa vipimo mara mbili, matokeo yalionesha ameathirika.
Kwa sababu hiyo, Hamilton ameshajitenga na timu yake. Siku ya Jumapili, Hamilton alishinda mbio za 11 kwa mwaka huu baada ya kuibuka kidedea kwenye mbio za Bahrain Grand Prix.
Taarifa rasmi kutoka Mercedes imeandikwa “Mbali na kuonesha dalili, [Hamilton] yupo vizuri na timu nzima inamtumia salamu za kumtakia afya njema”
Mercedes bado hawajamtaja dereva atakayeziba pengo la Hamilton kwenye mbio za Sakhir GP wikiendi hii na wamesema mchakato huo utafanyika muda wowote kuanzia sasa.
Kukosekana kwenye mbio za Sakhir GP itakuwa ni mara ya kwanza kwa Lewis Hamilton kukosekana uwanjani tangu alipoanza kucheza F1 mwaka 2007.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
warda
Ahaaaa hii corona sasa mashindano hyanogi tena bila Lewis
Issa
Covid ni shida sana
Sarah
Pole yake
Carolina
Corona sa Ivi imehamia kwa wachezaji
Magdalena
Huu ugonjwa ni balaa
Tatu
Corona Bado tishio
Lydia Emmanuel Magoti
Daa pole yake
Hopemwaikuka
Get well soon my fav champ
Nasra
Corona sio poa
aisha
Corona imekua nitishio
Sabrina
Corona hii nishidah
felister
corona bado ni tishio
Ester jackson
Corona bado ni tishio
samiah
Corona tishio bado
Zainabu kihongosi
Nachukua huu ugonjwa