Lewis Hamilton Kuikosa Sakhir GP.

Habari mbaya kwa wapenzi wa mbio za magari ya Formula 1 (F1), bingwa wa dunia – Lewis Hamilton amekutwa na maambukizi ya COVID19 na atakosa mbio za Sakhir GP wikiendi hii.

Taarifa hii imeripotiwa baada ya timu ya Mercedes kuripoti kuwa Lewis Hamilton alianza kuonesha dalili za mgonjwa wa COVID19 na baada ya kufanyiwa vipimo mara mbili, matokeo yalionesha ameathirika.

Kwa sababu hiyo, Hamilton ameshajitenga na timu yake. Siku ya Jumapili, Hamilton alishinda mbio za 11 kwa mwaka huu baada ya kuibuka kidedea kwenye mbio za Bahrain Grand Prix.

Hamilton baada ya kushinda mbio za Bahrain Grand Prix wikiendi iliyopita.

Taarifa rasmi kutoka Mercedes imeandikwa “Mbali na kuonesha dalili, [Hamilton] yupo vizuri na timu nzima inamtumia salamu za kumtakia afya njema”

Mercedes bado hawajamtaja dereva atakayeziba pengo la Hamilton kwenye mbio za Sakhir GP wikiendi hii na wamesema mchakato huo utafanyika muda wowote kuanzia sasa.

Kukosekana kwenye mbio za Sakhir GP itakuwa ni mara ya kwanza kwa Lewis Hamilton kukosekana uwanjani tangu alipoanza kucheza F1 mwaka 2007.


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

15 Komentara

    Ahaaaa hii corona sasa mashindano hyanogi tena bila Lewis

    Jibu

    Covid ni shida sana

    Jibu

    Pole yake

    Jibu

    Corona sa Ivi imehamia kwa wachezaji

    Jibu

    Huu ugonjwa ni balaa

    Jibu

    Corona Bado tishio

    Jibu

    Daa pole yake

    Jibu

    Get well soon my fav champ

    Jibu

    Corona sio poa

    Jibu

    Corona imekua nitishio

    Jibu

    Corona hii nishidah

    Jibu

    corona bado ni tishio

    Jibu

    Corona bado ni tishio

    Jibu

    Corona tishio bado

    Jibu

    Nachukua huu ugonjwa

    Jibu

Acha ujumbe