Lewis Hamilton Kubadili Jina la Ukoo

Bingwa mara saba wa mashindano ya F1 Lewis Hamilton amefichua siri kuwa anampango wa kubadili  jina lake la koo na kuongeza jina la mama yake kwenye jina la ukoo.

Lewis Hamilton alimwalika mama yake kumwangalia akipokea “knighthood” kutoka kwa mwana mfalme Charles kwenye kasri ya Windsor mwezi  December, pia amesema nia yake ya kujumuisha jina la mama yake, Larbalestier likiwa pamoja na Hamilton.

Lewis Hamilton
Lewis Hamilton

 

Hamilton wazazi wake kati ya mama yake na baba yake walitengana wakati akiwa na miaka miwili, akizungumza kwenye maandalizi ya msimu mpya wa F1 ambao unatarajiwa kuanza nchini Bahrain siku ya jumapili alinukuliwa alisema, “kiukweli najivunia jina la mama yangu.

“Jina la mama yangu ni Larbalestier na nakwenda kuliweka kwenye jina langu. Sielewi kwa nini watu wanapoana mwanamke anapoteza jina lake na kiukweli nataka jina la mama yangu liwe sambamba na jina la Hamilton.”

Alipoulizwa lini anatarajia kubadilisha jina Hamilton alijibu, “natumai hivi karibuni, Tunalifanyia kazi sasa.”

Lewis Hamilton sasa anafanya maadalizi y kushiriki kwenye msimu wa wake wa 16 ili kuweza kulipa kisasi cha msimu uliopita baada ya matokeao ya mwisho kuwa na utata na Max Verstappen kutangazwa mshindi wa mashindano hayo.


SHAOLIN FORTUNES 100 ONJA LADHA YA USHINDI

Maana ya ushindi mkubwa ipo hapa katika mchezo wa SHAOLIN FORTUNES 100 ndani ya kasino maridhawa za meridianbettz. Kwa dau dogo unashinda zaidi, unaweza kucheza mara nyingi uwezavyo huku ukifurahia ladha ya ushindi.

liverpool, Liverpool Kila Mtu Ashinde Mechi Zake., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.