Kuelekea msimu mpya wa Formula 1, mchezaji chipukizi Yuki Tsunoda amejiunga na timu ya Alpha Tauri. Sasa ni rasmi kijana huyu atashiriki Formula 1 msimu ujao.
Tsunoda alimaliza katika nafasi ya 3 kwenye mbio za Formula 2 akiwa na timu ya Red Bull ambayo ilikuwa ikifanya kazi na Honda kama washirika wao.
Kiongozi wa Alpha Tauri – Franz Tost amesema ” Mwaka huu kwenye F2, Yuki Tsunoda ameonesha mchanganyiko mzuri wa namna ya uendeshaji pamoja na uelewa mkubwa wa masuala ya kiufundi.
“Ninahakika atakuwa na mchango mkubwa kwenye timu yetu. Kwenye mbio 2 za majaribio (Imola na Yas Marina), amethibitisha yupo tayari kucheza Formula 1.”
Hii ni hatua kubwa kwa mchezaji chipukizi kama Tsunoda ambaye ni kijana wa miaka 20 pekee. Kwa Tsunoda ” kama ilivyo kwa madereva wengine, lilikuwa ni lengo langu kucheza Formula 1, nimefurahi sana kwa taarifa hii.
“Nimegundua nitakuwa nimebeba matumaini ya wajapani wengi ambao ni mashabiki wa F1 na nitajitahidi kuwapafuraha.”
Yuki Tsunoda anakuwa Mjapani wa kwanza kucheza F1 baada ya Kamui Kobayashi ambaye aliipeperusha bendera ya timu ya Toyota kwenye mbio mbili za mwishoni mwaka 2019.
Sauber na Caterham ni wajapani wengine ambao waliwahi kucheza mashindano ya Formula 1 katika historia ya mashindano hayo.
BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!
Hopemwaikuka
All ze best kijana
Dorophina
Kila lakheri yuki majukumu yanaendelea
Adelta
Kila la kheri
Issa
Dereva bora
Khadija
Kila la kheri
Saupha mohamed
Kila la kheri
Shakila mrope
Dereva bora
Fatuma kasomo
Gud news
neema hassan
Habari njema kwa mashabk
samiah
Safi
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Samira
All the best kwako
Rahma
Kila lakheri
Caroline
Safi sanaaa
felister
kila la kheri
Tatu
Kila la khery
Janeflora malisa
Safi
warda
Yuki ni mda alikuwa anatamani kujiunga na hii timu