Baada ya mshambuliaji Diego Costa kuamua kuondoka Atletico Madrid, majirani hawa wa Real Madrid walizirusha ndoano zao kule Ligue 1 wakimlenga Moussa Dembele wa Olympique Lyonnais.
Usajili wa Dembele utakuwa wa mkopo kwa nusu ya msimu uliobaki na kama mchezaji huyo ataonesha cheche zake na kuisaidia Atletico, basi atasalia Wanda Metropolitano kwa dau la euro milioni 35.
Akiwa amepachika goli 1 katika michezo 16 ya Ligue 1 aliyocheza mpaka sasa kwa msimu huu, Dembele alipachika magoli 24 katika michezo 46 (ya mashindano yote) aliyocheza msimu uliopita.
Akizungumzia usajili huo, kocha wa Atletico – Diego Simeone amenukuliwa akisema “mchakato (wa usajili) umefikia mahali pazuri. Tutathibitisha hilo (usajili wake).”
Atletico Madrid wanaendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa La Liga msimu huu baada ya kuwachakaza Sevilla kwa ushindi wa 2-0 jana usiku.
MERIDIANBET INAKUPA NAFASI YA KUWA MILIONEA KWA KILA BAADA YA DAKIKA 5
Mchezo wa Keno unakupatia fursa ya kuibuka kidedea kupitia droo zinazochezwa kila baada ya dakika 5 tu!! Tunaposema Meridianbet ni nyumba ya mabingwa, tunamaanisha!!
Caroline
Asante kwa taarifa
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana dembele
Rahmal
Safi sana dembele
Sadick
Usajiri makini. Familia ya dembele ina wachezaji wengi mahili
Sarah
Safi sana dembele
Sabrina
Inapendeza sana
Mwanahamisi
Safi sana
Angelina
Nice update
Adelta
Ndembele Yuko makini Sana
Dorophina
Dembele mchezaji ninaye mkubali sana
Magdalena
Dembele yuko poa
Hopemwaikuka
Namkubal sana
Neema juma
Inapendeza sana
Sania
Dembele yuko fiti
Saupha mohamed
Safi sana
warda
Imekaa poa