Morrison Kuikosa Dabi Kesho

NYOTA wa Yanga, Benard Morrison ataukosa mchezo wa kesho wa ligi kuu kati ya Yanga na Simba kutokana na adhabu anayoitumikia.

Dabi hiyo ya kariakoo itapigwa kesho jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar saa 11:00 jioni.

Akizungumzia maandalizi yao, Kocha Mkuu wa Yanga, Nassredine Nabi amesema kila kitu kipo sawa kuelekea kwenye huo mchezo lakini muhimu ni kupata ushindi.

“Wachezaji wote wapo fiti na maandalizi yetu yamekamilika, tunajua mchezo utakuwa mgumu lakini ni muhimu kupata ushindi kwenye huo mchezo.

“Tunawaheshimu sana wapinzani wetu ila tunatambua kitu gani ambacho wananchi wanahitaji kukiona, mchezaji ambaye tutamkosa ni Benard Morrison ambaye bado anatumikia adhabu.”


Unaweza kubashiri na Meridianbet kwa kupiga *149*10# kubashiri na Meridianbet! Au tembelea tovuti yetu kwa kubonyeza HAPA

Acha ujumbe