Mabingwa watetezi Real Madrid walikabwa koo na kulazimishiwa sare tasa na Real Sociedad katika mchuano wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) msimu huu.
Kikosi hicho cha kocha Zinedine Zidane kilianza kampeni zake wiki moja baada ya timu nyinginezo kwa kuwa kilishiriki soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mwezi uliopita.
Ingawa hivyo, walikosa kuridhisha matarajio ya mashabiki dhidi ya Sociedad na wakapata fursa chache sana za kufunga mabao.
Jaribio la kwanza la Real langoni pa wenyeji wao lilikuwa katika dakika ya 24 ila kombora lake likapanguliwa kirahisi na kipa Alex Remiro.
Mchuano huo ulikuwa wa kwanza kiungo na nahodha wa zamani wa Manchester City, David Silva, kushiriki tangu aingie katika sajili rasmi ya Sociedad.
Sociedad nao walipata nafasi nyingi za wazi ila wakazipoteza. Alexander Isak alisalia uso kwa uso na kipa Thibaut Courtois katika dakika ya 28, sekunde chache baada ya Ander Barrenetxea kupaisha mpira ambao vinginevyo ungewaweka waajiri wake kifua mbele.
Real Madrid walikosa huduma za kiungo Eden Hazard anayeuguza jeraha la kifundo cha mguu kwenye mechi hiyo.
Kuondoka kwa Gareth Bale aliyeyoyomea Tottenham Hotspur kwa mkopo kulitoa nafasi kwa washambuliaji chipukizi wazawa wa Brazil, Vinicius Junior na Rodrygo kushirikiana na Benzema katika safu ya mbele ya Real huku Martin Odegaard akitegemewa pakubwa katika safu ya kati.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.
Fatuma kasomo
Habari njema
Mwanahamisi
Gud news
felister
game ilikua ngumu sana kwa real
Theonestina
Habari njema
Salma ngende
Habari mbaya kwa mashabiki wao
Latifa juma mohamed
Game ilikuwa ngumu wajipange mechi zjazo.
Neema
naona mtanangee ulikuwa mgumu kweli kwa Real Madrid
Ernest
Sio jambo geni sana kwa kawaidia wachezaji wanapokuwa likizo huwa na kazi moja tu ya kurelax hivyo itachukua muda kidogo kurudi kwenye fomu
Elika
Kwa game ile sio poa kabisa
Lydia Emmanuel Magoti
Real Madrid sio wakulaumiwa ila mpila ukikataa uwezi kuhufosi kitu kiwezekane Game ilikuwa ngumu Sana wakati mwingine watajipanga vizuri
Adelta
Asante kwa makala nzuri@meridianbettz
Janeflora malisa
Mambo c mazur
magdalena
madrid wameanza na kutuvunja mioyo sisi mashabiki kwa kutoka sare zidi ya wapinzani wao
Angelina
Wajipange upya
Zeiyana
Hapo ndio zidane hatajua samani ya bale
Gabriel
wachezaji wanapokuwa likizo huwa na kazi moja tu ya kurelax hivyo itachukua muda kidogo kurudi kwenye form nzur sana
Tatu
Madrid walijisau sana naona mechi ijao watajipanga upya
Fatina
Wajipange tyu upya!
Shani
Madrid wana dharau sana timu ilo linawakosti mwishon
Mwajumah
Habari njema
Hopemwaikuka
Wajikaze mda bado upo
Hidaya
Habari mbaya kwa mashabiki wa soka
aisha
Duuh madrid wanakwama wapi majanga hayo
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
Mwajuma msangi
Mwanzo mgumu tu lakini mambo yatakaa sawa tu
Rehema
Gud news 👍
Khadija
Kwa mchezo hule sio poa kabisa
Sadick
Real Madrid haiwezi kutetea ubingwa endapo haitasajili wachezaji wapya, wapo bize kuuza kuliko kununua wachezaji#meridianbettz
Saupha mohamed
Real Madrid hawana wachezaji
Amiri Kayera
Mwanzo mbaya lakin wanamda wa kujipanga
Issa
Madrid inasua sua sana haiwez kudumu sna
Sabrina
Waswahili wanasema mwanzo mgumu ila sina mashaka na madrid watafanya vzuri tu
Tumaini kasalile
Dash majanga ila haina shida msimu ndo umeanza wajipange upya pamoja na kusajili mana dirisha bado halijafungwa
Dorophina
Madrid walijitahidi sana lakini haikuwa bahati yao gemu ilikuwa tafu sana
Samiah
Gud
Sauda
Wanatakiwa kijipanga
Rose kapinga
Mwanzo mgumu,jipangeni upya!!!
David Pere
Habari mbaya kwa mashabiki wao