Real Madrid Wameweka 'Stop' kwa Mbappe

Real Madrid wameripotiwa kuweka wazi kwa Paris Saint-Germain kwamba hawatachukua hatua zozote kwa Kylian Mbappe hadi mabingwa wa Ufaransa watakapokuwa tayari kumuuza.

Hatma ya kinda huyu wa miaka 22 huko Paris inabaki kuwa mada kwenye minong’ono mingi ya soka, na mkataba wake wa sasa kusalia kule Paris uko mbioni kumalizika katika msimu wa joto wa 2022.

Ripoti ya hivi karibuni ilidai kuwa Mbappe alikuwa tayari kusaini mkataba mpya wa muda mrefu na PSG kwa nia ya kujiungaa na mabingwa wa Uhispania ndani ya miaka miwili ijayo.

Klyian Mbappe

Real Madrid wanaonekana kutokuwa na uhakika wa kuwa na pesa zinazohitajika kupata saini ya nyota huyu wa kimataifa wa Ufaransa mwaka huu kutokana na athari za kifedha za baada ya mlipuko wa coronavirus.

Kwa mujibu wa Marca, uongozi katika wa Real Madrid umeamua rasmi kuwa hawatamfukuzia mshindi huyu wa Kombe la Dunia hadi PSG iwe tayari kuachana naye kwani kuna ‘heshima kubwa baina ya vilabu hivyo viwili’.

Mbappe, ambaye pia anaendelea kuhusishwa na Liverpool, amefunga mabao 107 katika mechi 149 katika mashindano yote kwa timu yake ya sasa tangu awasili kutoka Monaco.


TENGENEZA MKWANJA UKIWA NA MERIDIANBET 

Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye  kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.

SOMA ZAIDI

14 Komentara

    Real Madrid kuweni na subra mtampata tu

    Jibu

    Real Madrid haina uwezo wa kifedha kununua mchezaji wa bei kubwa kama Mbappe

    Jibu

    Kwa Mbape sidhan kama itawezekana

    Jibu

    Hao PSG Wanavyoringa na huyo mmbape wao

    Jibu

    Kwanini Sasa wanamuwekea kizuizi

    Jibu

    Madrid wawaachie wenye ela tu wambebe mbappe

    Jibu

    Naona PSG wanachelewesha deal la Mbappe kupiga mkwanja sababu utakuwa uhamisho kukata na shoka

    Jibu

    Hapo mchawi pesa tu

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Hapo wanambania Mbape kuchukua mkwanja

    Jibu

    duh

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Vizuri pesa ndio kila kitu

    Jibu

Acha ujumbe